Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Ezekieli 19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombolezo

1 Mungu aliniambia niimbe wimbo huu wa maombolezo juu ya wakubwa wa Waisraeli:

2 Mama yenu alikuwa simba mwenye utukufu kati ya simba wengine. Alikaa kati ya simba wakali, akawalisha watoto wake.

3 Alimulea mutoto mumoja kati ya watoto wake, mutoto huyo naye akakuwa simba mukali. Akajifunza toka kwa mama yake kuwinda, akakuwa simba mukula watu.

4 Mataifa yakatangaza habari ya hatari juu yake, wakamunasa katika mutego wao, wakamupeleka juu ya ndoana mpaka Misri.

5 Mama yake alipoona kwamba amechoka kungoja, matumaini ya kumupata yakakwisha, akamutwaa mutoto wake mwingine, akamufanya simba mukali.

6 Huyo alipokuwa amekwisha kukomaa, akaanza kutembea pamoja na simba wengine. Naye vilevile akajifunza kuwinda, akakuwa simba mukula watu.

7 Alishambulia nyumba za watu na kuiharibu miji yao. Inchi pamoja na wakaaji wake viliogopa, kwa sauti ya kunguruma kwake.

8 Mataifa yakamushambulia kutoka pande zote, wakatandaza wavu wao juu yake, naye akanaswa katika mutego wao.

9 Kwa ndoana wakamutia katika kizimba chao, wakamupeleka kwa mufalme wa Babeli. Kule, wakamutia katika kifungo, kusudi ngurumo yake isisikilike tena juu ya milima ya Waisraeli.

10 Mama yako alikuwa kama muzabibu katika shamba, uliopandikizwa pembeni ya maji, ambao ulizaa sana kwa kuwa na maji mengi.

11 Ulikuwa na matawi yenye nguvu, ambayo yalikuwa fimbo za kifalme. Muzabibu huo ulikomaa kupita miti mingine, watu walisifu ukubwa wa shina lake na wingi wa matawi yake.

12 Lakini uliongolewa kwa hasira, ukatupwa chini juu ya udongo; upepo mukali wa mashariki ukaukausha, matunda yake yakaanguka; matawi yake yenye nguvu yalikauka, nao moto ukauteketeza.

13 Na sasa umepandikizwa katika jangwa, katika inchi yenye kukauka isiyokuwa na maji.

14 Lakini moto umetoka kwenye shina lake, ukayateketeza matawi na matunda yake. Matawi yake hayatakuwa na nguvu hata kidogo, wala hayatakuwa fimbo za kifalme. Huo umekuwa wimbo wa maombolezo; ndivyo unavyoimbwa siku zote.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan