Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Danieli 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Rafiki za Danieli wanashitakiwa

1 Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi katika raha na amani katika nyumba yangu ya kifalme.

2 Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala katika kitanda, mawazo na maono yaliniogopesha.

3 Hivyo, nikaamuru wenye hekima wote wa Babeli waletwe mbele yangu kusudi wanielezee maana ya ndoto hiyo.

4 Halafu waganga, walozi, Wakaldea na wenye hekima wakaletwa. Nikawaelezea ndoto yangu, lakini hawakuweza kunieleza maana yake.

5 Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:

6 Ee Beltesaza, unayekuwa mukubwa wa waganga, ninafahamu kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba hakuna fumbo linalokuwa gumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu; uniambie maana yake.

7 Nilipokuwa ninalala, niliona maono haya: Niliona muti murefu sana katikati ya dunia.

8 Muti uliendelea kukomaa, ukakuwa imara na kilele chake kikafika mbinguni. Uliweza kuonekana kutoka kila pahali katika dunia.

9 Majani yake yalikuwa mazuri. Ulikuwa umejaa matunda mengi yaliyotoshelea kwa kulisha dunia nzima. Nyama wote wa pori walipata kivuli chini yake, na ndege wa anga walikaa katika matawi yake. Viumbe vyote vilipata chakula kutoka muti huo.

10 Nilipokuwa ninalala katika kitanda, niliona maono: Mulinzi mutakatifu alishuka kutoka mbinguni.

11 Akalalamika kwa sauti akisema: Mukate muti huu na kuyakatakata matawi yake. Muangushe majani yake na kuyatawanya matunda yake. Nyama wakimbie toka chini yake na ndege kutoka matawi yake.

12 Lakini muache kisiki chake na mizizi yake ndani ya udongo, kwenye majani mabichi ndani ya shamba kikiwa kimefungwa pale kwa munyororo wa chuma na shaba. Muache kilowanishwe na umande wa mbinguni; muache kiishi pamoja na nyama wa pori na kula majani katika mbuga.

13 Akili yake ya kimutu ibadilishwe, akuwe na akili ya nyama kwa miaka saba.

14 Hii ni hukumu iliyotangazwa na walinzi; ni uamuzi wa wanaokuwa watakatifu, kusudi wanadamu wote kila pahali wapate kutambua kwamba Mungu Mukubwa ana mamlaka juu ya falme zote za wanadamu; yeye anamupatia ufalme mutu yeyote anayemupenda, anamufanya kuwa mufalme hata mutu muzaifu wa mwisho.

15 Hii ndiyo ndoto niliyoota mimi Nebukadneza. Sasa, wewe Beltesaza, unielezee maana yake; maana wenye hekima wote katika ufalme wangu hawawezi kuniambia maana yake; lakini wewe utaweza kwa maana roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako.


Danieli anaeleza maana ya ndoto

16 Basi, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, akashangaa kwa muda, na mafikiri yake yakamufazaisha. Mufalme akamwambia: Beltesaza, ndoto hii, wala maana yake visikufazaishe! Beltesaza akamujibu: Bwana wangu, ingelikuwa heri ndoto hii na maana yake iwaelekee waadui zako!

17 Muti uliouona ukiwa mukubwa na wenye nguvu, ambao matawi yake marefu yalifika mbinguni, nao ukionekana kutoka kila pahali katika dunia,

18 majani yake yakiwa mazuri, na matunda yake mengi ya kukulisha viumbe vyote, nyama wa pori wakipata kivuli chini yake, na ndege wakikaa katika matawi yake,

19 basi, ni wewe, ee mufalme, ambaye umekuwa mukubwa na mwenye nguvu. Ukubwa wako umefika mpaka mbinguni, na ufalme wako umeenea mpaka miisho ya dunia.

20 Kisha ukaona tena, ee mufalme, Mulinzi mutakatifu akishuka kutoka mbinguni, akaamuru: Mukate muti huu, muuangamize. Lakini muache kisiki chake na mizizi yake katika udongo kwenye majani mabichi ya mashamba, kikiwa kimefungwa pale kwa munyororo wa chuma na shaba. Muache kilowanishwe na umande wa mbinguni; muache kiishi pamoja na nyama wa pori kwa miaka saba.

21 Hii basi, bwana wangu, ndiyo maana ya ndoto yako, kadiri ya uamuzi wa Mungu Mukubwa juu yako:

22 Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu. Utaishi pamoja na nyama wa pori, utakula majani kama ngombe; utalowana na umande wa mbinguni. Utakaa katika hali hiyo kwa miaka saba, na kwa mwisho utatambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya ufalme wa wanadamu naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.

23 Tena amri ile ya kukiacha kisiki na mizizi ya muti huo katika udongo ina maana hii: Wewe utarudishiwa tena ufalme wako wakati utakapotambua kwamba Mungu wa mbinguni ndiye anayetawala.

24 Kwa sababu hiyo, ee mufalme, sikiliza shauri langu. Achana na zambi zako na maovu yako, utende haki na kuwaonea huruma walioteswa; labda muda wako wa kufanikiwa utarefushwa!


Maana ya ndoto inatimia

25 Hayo yote yalimupata mufalme Nebukadneza.

26 Nyuma ya miezi kumi na miwili, mufalme Nebukadneza alikuwa anatembea juu ya dari ya nyumba ya kifalme katika muji wa Babeli.

27 Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!

28 Alipokuwa angali anasema maneno hayo, sauti kutoka mbinguni ikamwambia: Ewe mufalme Nebukadneza, sikiliza ujumbe huu juu yako! Umenyanganywa ufalme!

29 Utafukuzwa mbali na wanadamu! Utaishi pamoja na nyama wa pori, na utakula majani kama ngombe! Utakaa katika hali hiyo kwa miaka saba, na kwa mwisho utatambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye mwenye uwezo juu ya falme za wanadamu, na anamupa ufalme mutu yeyote anayemutaka.

30 Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Nebukadneza anamusifu Mungu

31 Kwa mwisho wa ile miaka saba, mimi Nebukadneza niliinua macho yangu kuangalia juu mbinguni na akili zangu zikanirudilia. Nilimushukuru Mungu Mukubwa na kumuheshimu yeye anayeishi milele: Kwa sababu mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ufalme wake unadumu kwa vizazi vyote.

32 Wakaaji wote wa dunia si kitu; anafanya anavyotaka na viumbe vya mbinguni, na wakaaji wa dunia; hakuna anayeweza kumupinga, au kusema: Unafanya nini?

33 Wakati uleule akili zangu zikanirudilia; nilirudishiwa vilevile heshima yangu, mamlaka yangu na utukufu wa ufalme wangu. Washauri na wakubwa wangu walikuja kunitafuta, nikarudishwa katika ufalme wangu na kupata heshima kama pale mbele.

34 Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan