Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Danieli 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Nebukadneza anasimamisha sanamu Mufalme anamutolea Danieli zawadi

1 Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.

2 Kisha mufalme akaamuru maliwali, wasimamizi, watawala, washauri, walinzi wa mali, waamuzi, wana sheria na wakubwa wote wa majimbo wahuzurie sikukuu ya kuzindua sanamu aliyosimamisha.

3 Basi, maliwali, wasimamizi, watawala, washauri, walinzi wa hazina, wana sheria na wakubwa wote wa majimbo wakakusanyika tayari kwa muzinduo wa sanamu mufalme Nebukadneza aliyosimamisha.

4 Mutangazaji wa habari akatangaza kwa sauti kubwa: Enyi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote, munaamuriwa kwamba

5 mukisikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, munapaswa kuinama chini na kuabudu sanamu ya zahabu mufalme Nebukadneza aliyosimamisha.

6 Na yeyote ambaye hatainama chini na kuiabudu, atatupwa mara moja katika furu la moto mukali.

7 Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.

8 Wakati huo, watu wamoja kati ya Wakaldea wakajitokeza na kuwashitaki Wayuda. Walimwambia mufalme Nebukadneza:

9 Uishi milele, ee mufalme!

10 Wewe, ee mufalme, ulitoa amri kwamba kila mutu anaposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na kila aina ya muziki, ainame chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu.

11 Na kwamba mutu yeyote asiyeinama chini na kuiabudu sanamu hiyo, atupwe ndani ya furu la moto mukali.

12 Sasa, kuna Wayuda fulani uliowachagua kwa kushugulikia mambo ya utawala wa jimbo la Babeli, nao ni: Sadiraki, Mesaki na Abedenego; watu hawa, ee mufalme, hawakutii amri yako. Wanakataa kuitumikia miungu yako na kuiabudu ile sanamu ya zahabu uliyoisimamisha.

13 Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.

14 Mufalme Nebukadneza akawauliza: Ni kweli kwamba wewe Sadiraki, wewe Mesaki na wewe Abedenego, hamwitumikii miungu yangu wala kuiabudu ile sanamu ya zahabu niliyoisimamisha?

15 Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?

16 Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakamujibu mufalme: Ee Nebukadneza, sisi hatuhitaji kukujibu juu ya jambo hilo.

17 Mungu wetu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Atatuokoa kutoka furu la moto mukali na vilevile kutoka katika mikono yako, ee mufalme.

18 Lakini, hata kama haitafanyika hivyo, ujue wazi, ee mufalme, kwamba sisi hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya zahabu uliyosimamisha.


Wenzake na Danieli wanahukumiwa

19 Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.

20 Akaamuru watu fulani wenye nguvu kabisa kati ya waaskari wake wawafunge Sadiraki, Mesaki na Abedenego na kuwatupa katika ile furu ya moto mukali.

21 Basi, vijana hao wakafungwa wakiwa wamevaa makoti yao, kanzu zao, kofia na nguo zao zingine, wakatupwa katikati ya ile furu la moto mukali.

22 Kwa vile amri ya mufalme ilikuwa kali, ule moto ulikuwa umewashwa na kuwa mukali sana, hata ndimi za moto zikawateketeza wale watu waliowapeleka Sadiraki, Mesaki na Abedenego.

23 Halafu Sadiraki, Mesaki na Abedenego, wakiwa wamefungwa, wakatumbukia katika ile furu ya moto mukali.

24 Basi, mufalme Nebukadneza akashangaa, akasimama kwa haraka na kuwauliza washauri wake: Si tuliwafunga watu watatu na kuwatupa katika moto? Nao wakamujibu mufalme: Kweli, mufalme! Ndivyo!

25 Kisha akauliza: Lakini sasa mbona ninaona watu wane wakitembeatembea mule ndani ya moto bila kufungwa na wala hawaunguwi, na mutu wa ine anaonekana kama mwana wa miungu?


Vijana wanaachwa huru

26 Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.

27 Maliwali, wasimamizi, wakubwa wa majimbo na washauri wa mufalme, wote wakakusanyika pamoja, wakaona kwamba ule moto haukuweza kuwaunguza hao watatu. Nywele zao hazikuungua, nguo zao hazikuungua wala hawakuwa na harufu yoyote ya moto.

28 Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.

29 Kwa hiyo, ninaamuru kwamba watu wa kabila lolote, taifa lolote au luga yoyote, watakaosema kitu chochote cha kumuzarau Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watakatwa vipandevipande na nyumba zao zitabomolewa. Maana hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa namna hii.

30 Basi, mufalme Nebukadneza akawapandishia vyeo Sadiraki, Mesaki na Abedenego katika jimbo la Babeli.


Ndoto ya pili ya mufalme Nebukadneza

31 Mufalme Nebukadneza aliwaandikia hivi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote katika dunia: Ninawatakia amani tele!

32 Nimeona vema kuwajulisha kitambulisho na maajabu ambayo Mungu Mukubwa amenionyesha.

33 Kweli vitambulisho vya Mungu ni kubwa! Maajabu yake ni makubwa sana! Ufalme wake ni ufalme wa milele; ufalme wake unadumu kwa vizazi vyote.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan