Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Danieli 10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maono ya Danieli kando ya muto Tigre

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.

2 Wakati huo, mimi Danieli, nilikuwa nikiomboleza kwa muda wa majuma matatu.

3 Sikukula chakula kizuri, sikugusa nyama wala divai, na sikujipakaa mafuta kwa muda wa majuma hayo yote matatu.

4 Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi wa kwanza, nilikuwa nimesimama kando ya muto Tigre.

5 Nikainua macho, nikamwona mutu anayevaa nguo za kitani naye alikuwa amejifunga mukaba wa zahabu safi kutoka Ufasi.

6 Mwili wake ulingaa kama zabarajadi safi. Uso wake ulifanana na umeme, na macho yake yaliwaka kama ndimi za moto. Miguu na mikono yake ilingaa kama shaba iliyosafishwa sana. Sauti yake ilivuma kama sauti ya kundi kubwa la watu.

7 Mimi Danieli peke yangu niliona maono hayo. Wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini walishikwa na hofu sana, wakakimbia, wakajificha.

8 Hivyo, niliachwa peke yangu nikiangalia hayo maono ya kushangaza. Nguvu zikaniishia, na uso wangu ukabadilika rangi, nikabaki bila nguvu.

9 Nilipoisikia sauti yake, nilianguka uso mpaka chini, nikashikwa na usingizi muzito.

10 Hapo, mukono ukanigusa, ukanisimamisha, na kuimarisha miguu na mikono yangu.

11 Akaniambia: Danieli, wewe unayependwa sana, simama sawa usikilize kwa uangalifu maneno nitakayosema, maana nimetumwa kwako. Alipokuwa akiniambia maneno haya, mimi nilisimama nikitetemeka.

12 Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.

13 Mukubwa wa ufalme wa Persia alinipinga kwa muda wa siku makumi mbili na moja. Lakini Mikaeli, mumoja kati ya wakubwa, akakuja kunisaidia, kwa hiyo nikamwacha kule pamoja na mukubwa wa ufalme wa Persia,

14 nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.

15 Alipokuwa ananiambia maneno hayo, niliangalia chini bila kuweza kusema.

16 Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.

17 Mimi ni kama mutumwa mbele ya bwana wake. Ninaweza namna gani kusema nawe? Sina nguvu na pumzi imeniishia!

18 Yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa kwa mara ingine, akanitia nguvu.

19 Akaniambia: Usiogope wewe unayependwa sana, uko salama. Ukuwe imara na hodari. Aliposema nami, nilipata nguvu, nikamwambia: Bwana, umekwisha kuniimarisha; sema kile ulichotaka kusema.

20 Naye akaniambia: Unajua kwa nini nimekuja kwako? Sasa ninapaswa kurudi kwenda kupigana na malaika mulinzi wa Persia. Halafu, nitakapokuwa nimemushinda, malaika mulinzi wa mufalme wa Ugriki atatokea.

21 Lakini nitakujulisha yale yaliyoandikwa katika kitabu cha ukweli. Sina mwingine wa kunisaidia kwa kuwashinda hawa isipokuwa Mikaeli, malaika mulinzi wenu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan