Amosi 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maono ya ine: Kikapu cha matunda 1 Bwana wetu Yawe alinionyesha maono mengine: Niliona kikapu kilichojaa matunda yenye kuivya. 2 Naye Yawe akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kikapu cha matunda yenye kuivya. Kisha Yawe akaniambia: Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli. Sitavumilia tena maovu yao. 3 Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya. Mungu ataiazibu Israeli 4 Musikilize, enyi munaowagandamiza wakosefu na kuwaletea maangamizi wamasikini wa inchi. 5 Munajisemesha ndani ya mioyo yenu: Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu? Siku ya Sabato itakwisha wakati gani kusudi tupate kuuzisha ngano yetu? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa. 6 Tutawanunua wamasikini kwa feza na wakosefu kwa bei ya muguu mumoja wa mapapa. Nasi tutauzisha machenga ya ngano. 7 Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa: Hakika, sitayasahau matendo yao maovu. 8 Kwa hiyo, dunia itatetemeka na kila mutu katika inchi atafanya kilio. Inchi yote itayumbayumba; itapanda na kushuka, kama vile maji ya muto Nili yanavyojaa na kupunguka! 9 Siku hiyo, nitalifanya jua litue pa saa sita za muchana, na kuijaza inchi giza wakati wa muchana. –Ni ujumbe wa Yawe.– 10 Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa. 11 Siku zinakuja ambapo nitaleta njaa katika inchi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Lakini si njaa ya kukosa chakula wala kiu ya kukosa maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Yawe. 12 Watu watatangatanga kutoka bahari hata bahari, kutoka upande wa kaskazini mpaka wa mashariki. Watakimbia huko na huko wakitafuta neno la Yawe, lakini hawatalipata. 13 Siku hiyo, wabinti wazuri na vijana wanaume watazimia kwa kiu. 14 Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo