Amosi 5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombolezo ya Amosi 1 Musikilize maombolezo yangu juu yenu, enyi Waisraeli: 2 Umeanguka na hautainuka tena ewe binti Israeli! Umeachwa ukiwa katika inchi yako, hakuna hata mutu wa kukuinua. 3 Maana Bwana wetu Yawe anasema: Itakuwa hivi: juu yenu ninyi Waisraeli: Watu elfu moja wanatoka katika muji kwenda kupigana lakini watarudia watu mia moja tu; wataondoka watu mia moja wa kijiji kimoja lakini watu kumi tu wataponyoka. 4 Yawe anawaambia Waisraeli hivi: Munitafute mimi nanyi mutaishi! 5 Lakini musinitafutie kule Beteli wala musiende Gilgali wala musivuke kwenda Beri-Seba. Maana wakaaji wa Gilgali, hakika watapelekwa katika uhamisho, na Beteli utaangamizwa! 6 Mutafute Yawe, nanyi mutaishi! Kama sivyo, atawatokea wazao wa Yosefu kama moto; moto utawateketeza wakaaji wa Beteli na hakuna mutu atakayeweza kuuzimisha. 7 Angalisho, enyi munaogeuza sheria kuwa uchungu, na kuona haki kuwa kama takataka! 8 Huyo aliyezifanya nyota zinazoitwa Kilimia na Orioni, ambaye analigeuza giza nene kuwa muchana, na muchana kuwa usiku; yeye anayekusanya maji ya bahari na kuyamwanga juu ya inchi kavu, Yawe ndilo jina lake. 9 Yeye ndiye anayewaangamiza wenye nguvu, na kuziharibu kuta zao zenye nguvu. 10 Ninyi munawachukia wanaotetea haki na wenye kusema ukweli katika tribinali. 11 Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake. 12 Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali. 13 Basi, kutakuwa wakati mubaya ambao hata mwenye hekima atanyamaza. 14 Mutafute kutenda mazuri wala si mabaya, kusudi ninyi mupate kuishi naye Yawe wa majeshi atakuwa pamoja nanyi kama vile munavyosema. 15 Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki. 16 Basi, Yawe, Mungu wa majeshi, Bwana wetu anasema hivi: Kutakuwa kilio kila nafasi katika barabara za muji; watu wataomboleza: Ole! Ole! Walimaji wataitwa kuja kuomboleza, na wafundi wa kuomboleza kuja kufanya kilio. 17 Kutakuwa kilio katika mashamba yote ya mizabibu; maana nitapita kati yenu kwa kuwaazibu. Ni Yawe anayesema hivyo. Siku ya Yawe 18 Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu siku ya Yawe! Kwa nini munaitaka sana siku hiyo? Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza! 19 Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba, halafu anakutana na dubu! Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake, na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka. 20 Siku ya Yawe itakuwa giza, na si mwangaza; itakuwa giza kubwa bila mwangaza wowote. 21 Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini. 22 Hata mukinitolea sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na za vyakula, mimi sitakubali kuzipokea; na sadaka zenu za amani za nyama wanono mimi sitaziangalia kabisa. 23 Muondoe mbele yangu kelele za nyimbo zenu! Sitaki kusikiliza muziki wa vinubi vyenu! 24 Lakini muache haki itiririke kama maji, usawa ukuwe kama muto usiokauka. 25 Enyi Waisraeli, wakati ule mulipokuwa kule katika jangwa kwa miaka makumi ine, muliniletea matoleo na sadaka hata mara moja? 26 Mulibeba kama vile sasa sanamu za mungu wenu Sakuti mufalme wenu na sanamu za Kiuni mungu wenu wa nyota, vitu ambavyo mulijitengenezea wenyewe? 27 Kwa hiyo nitawapeleka katika uhamisho, mbali kuliko Damasiki! –Ni Yawe anayesema, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo