Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Amosi 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:

2 Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Madaraka ya nabii

3 Watu wawili wanaweza kusafiri pamoja bila kupatana kwanza?

4 Simba ananguruma katika pori kama hajapata nyama? Simba mukali ananguruma katika pango lake kama hajakamata kitu?

5 Mutego bila chambo utamunasa ndege? Mutego unaweza kufyatuka bila kuguswa na kitu?

6 Baragumu ya vita inalia katika muji bila kutia watu hofu? Muji unaweza kupatwa na hasara ambayo haikuletwa na Mungu?

7 Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.

8 Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Kuangamizwa kwa Samaria

9 Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.

10 Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.

11 Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waadui wataizunguka inchi yenu, wataharibu kuta zako, na kuziteka nyumba zao nzuri.

12 Yawe, anasema hivi: Kama vile muchungaji anavyonyanganya toka katika kinywa cha simba miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watu wachache tu wa Israeli wanaoishi Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri watakavyobaki.

13 Musikilize, muwaonye wazao wa Yakobo. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, Mungu wa majeshi.–

14 Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.

15 Nitaziharibu nyumba zote katika muji na katika vijiji; nitazibomoa nyumba zilizopambwa kwa pembe za tembo, nyumba kubwakubwa zitaanguka. –Ni ujumbe wa Yawe.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan