Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

2 Wakorinto 9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kusaidia wandugu

1 Si lazima niwaandikie juu ya musaada unaotumwa kwa watu wa Mungu wanaokuwa katika Yudea.

2 Kwa maana ninajua nia yenu nzuri ya kusaidia, nami ninajivuna kwa ajili yenu mbele ya watu wa Makedonia, nikisema: “Kanisa la jimbo la Akaya liko tayari kusaidia tangia mwaka jana.” Hivi kwa njia ya bidii yenu mumewavuta wengi kati yao kwa kutoa vilevile.

3 Lakini sasa ninawatumia wandugu hawa kusudi kujisifu kwetu kwa ajili yenu kusionekane kuwa bure. Kwa hiyo ninataka mukuwe tayari kama vile nilivyosema.

4 Kwa maana kama watu wa Makedonia wanakuja pamoja nami na tusipowakuta tayari, sisi tutapata haya sana kwa kuona jinsi nilivyowaaminia, nami sisemi kitu juu ya haya ambayo ninyi mutaweza kupata.

5 Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.

6 Mukumbuke maneno haya: yule anayepanda kidogo atavuna kidogo, na yule anayepanda kwa uwingi atavuna kwa uwingi.

7 Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.

8 Na Mungu anaweza kuwajalia mema ya kila namna, kusudi siku zote mupate vyote munavyohitaji, na hivi mupate kuzidi kutoshelewa katika kutenda kazi njema.

9 Kama vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ametoa kwa uwingi, amewapa wamasikini. Haki yake inadumu milele.”

10 Mungu ndiye anayemupatia mupandaji mbegu na mukate wa kukula. Kwa hiyo atawapatia ninyi mbegu yoyote munayohitaji na kuiotesha, kusudi moyo wenu wa kutoa upate kuzaa matunda mengi.

11 Hivi mutakuwa watajiri katika vitu vyote, kusudi siku zote muweze kuonyesha moyo wa kutoa, hata watu wengi watamushukuru Mungu kwa ajili ya musaada tunaowafikishia kutoka kwenu.

12 Kwa maana kazi hii ya kutoa munayofanya haifai tu kwa kusaidia watu wa Mungu kusudi wapate vitu wanavyokosa, lakini vilevile kwa njia ile watu wengi wanamutolea Mungu shukrani.

13 Kufuatana na ushuhuda wa kazi hii, watu watamutukuza Mungu kwa kuona jinsi munavyoonyesha utii wenu katika kushika Habari Njema ya Kristo. Vilevile wanamutukuza kwa kuona moyo wa kutoa munaokuwa nao katika kushirikiana mali yenu pamoja nao na sisi.

14 Kwa hiyo watawaombea kwa upendo mwingi, kwa ajili ya neema kubwa sana Mungu aliyowajalia.

15 Shukrani kwa Mungu kwa ajili ya zawadi yake inayopita kipimo!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan