Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

2 Wakorinto 13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maonyo ya mwisho na salamu

1 Hii ni safari yangu ya tatu ninayotayarisha kuja kwenu. Kama Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila neno linapaswa kuhakikishwa kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.”

2 Kwa wakati huu ninapokuwa mbali nanyi, ninarudilia kuwaambia waziwazi maneno yale niliyokuwa nimekwisha kuwaambia mbele katika safari yangu ya pili niliyofanya kwenu. Ninawaambia kwamba nitakapokuja kwenu mara tena, sitakosa kuazibu wale waliofanya zambi zamani na wengine wote.

3 Nitafanya vile kwa sababu ninyi munataka uhakikisho kwamba Kristo anasema kwa njia yangu. Kwenu Kristo si zaifu, lakini anaonyesha uwezo wake kati yenu.

4 Ni kweli Kristo alitundikwa juu ya musalaba katika hali ya uzaifu wa mwili, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Nasi katika kuungana kwetu naye sisi vilevile tunakuwa zaifu. Lakini kwa ajili yenu tunaishi pamoja naye kwa nguvu ya Mungu.

5 Mujichunguze ninyi wenyewe kusudi mupate kujua kama munasimama imara katika imani. Mujipime. Si munajua kwamba Yesu Kristo anakaa kati yenu? Kama si vile ni kusema kwamba mumeshindwa.

6 Lakini ninatumaini kwamba ninyi mutajua kwamba sisi hatukushindwa.

7 Nasi tunaomba Mungu kusudi musifanye jambo lolote baya, nasi hatutaki kuonyesha kwamba tumeshinda. Lakini tunataka mutende mema hata ikionekana kuwa sisi tunashindwa.

8 Kwa maana hatuwezi kufanya jambo lolote linalopingana na ukweli. Jambo tunaloweza tu ni kuendelesha ukweli.

9 Tunafurahi wakati ninyi munapokuwa na nguvu, hata ikiwa sisi ni zaifu. Nasi tunawaombea kusudi mupate kuwa wakamilifu.

10 Ni kwa hiyo ninawaandikia maneno haya nikiwa mbali nanyi, kusudi wakati nitakapokuwa kati yenu nisitende kwa ukali kadiri ya mamlaka Bwana aliyonipa. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.

11 Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.

12 Musalimiane kwa upendo wa kikristo. Watu wote wa Mungu wanawasalimia.

13 Tunawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu na ushirika wa Roho Mutakatifu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan