Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

2 Mambo ya Siku 4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Vifaa vya hekalu
( 1 Fal 7.23-51 )

1 Mufalme Solomono alitengeneza birika la maji la muviringo lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano na upana sawa na metre kenda, na urefu wake kwenda juu metre ine na nusu.

2 Kisha, akatengeneza birika la maji la muviringo, lenye upana wa metre ine na nusu kutoka ukingo mpaka ukingo, lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na lenye muzunguko wa metre kumi na tatu na nusu.

3 Chini ya ukingo wake, kuzunguka lile birika, kulikuwa mistari miwili ya sanamu za ngombe dume, kwa metre kumi na tatu na nusu. Sanamu hizo za ngombe dume zilikuwa zimetengenezwa na shaba ileile wakati birika lilipofanywa.

4 Nalo birika lilikuwa limewekwa juu ya sanamu za ngombe dume kumi na wawili, tatu zikielekea upande wa kaskazini, tatu upande wa magaribi, tatu kusini na zingine tatu upande wa mashariki.

5 Unene wa ukingo wake ulikuwa sentimetre saba na nusu. Ukingo wake ulikuwa kama ukingo wa kikombe, na kama maua ya yungiyungi. Ndani ya birika lile kuliweza kuingia kadiri ya litre elfu makumi sita za maji.

6 Akatengeneza vilevile beseni kumi za kusafishia sehemu za nyama zilizotumika katika sadaka za kuteketezwa kwa moto. Tano kati ya bakuli zile akaziweka upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Birika lilitumiwa na makuhani kwa kunawia.

7 Alitengeneza vinara kumi vya zahabu kama vile ilivyoagizwa, akaviweka katika baraza ya hekalu; vitano upande wa kusini, na vitano upande wa kaskazini.

8 Akatengeneza vilevile meza kumi, nazo akaziweka ndani ya chumba cha hekalu. Kisha akatengeneza beseni mia moja za zahabu.

9 Akatengeneza kiwanja cha ndani cha makuhani na kingine kikubwa cha inje, na milango ya kiwanja ambayo aliifunika na shaba;

10 na lile birika akaliweka kwenye pembe ya kusini-mashariki ya nyumba.

11 Hiramu akatengeneza vyungu, vipao na mabeseni. Basi Hiramu akamaliza kazi aliyomufanyia mufalme Solomono juu ya nyumba ya Mungu;

12 nguzo mbili, mabakuli, taji mbili juu ya nguzo, na nyavu mbili kwa ajili ya kufunika mabakuli ya taji zilizowekwa juu ya nguzo;

13 vilevile mifano ya makomamanga mia ine kwa ajili ya nyavu zile mbili, mistari miwili miwili ya makomamanga kwa kila wavu, kwa kupamba mabakuli yale mawili ya taji zilizokuwa juu ya kila nguzo.

14 Vilevile akatengeneza beseni juu ya magari,

15 na birika lile moja, na sanamu za ngombe dume kumi na wawili chini ya birika lile.

16 Halafu vyungu, vipao na kanya na vyombo vingine vyote vya nyumba ya Yawe ambavyo Huruma-Abi alimutengenezea mufalme Solomono, vilikuwa vya shaba iliyoangarishwa.

17 Vitu hivyo vyote mufalme alivitengeneza katika kiwanja cha Yordani, sehemu ya udongo wa mufinyanzi iliyokuwa kati ya Sukoti na Sereda.

18 Uzito wa shaba iliyotumiwa kwa kutengeneza vyombo hivi haukujulikana kwa maana Solomono alitengeneza vyombo vingi sana.

19 Solomono alitengeneza vitu vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu: mazabahu ya zahabu na meza za mikate mitakatifu;

20 vinara na taa za zahabu safi za kuangazia Pahali pale Patakatifu Sana, kama vile walivyoamuriwa;

21 maua, taa na koleo, vyote vikiwa vya zahabu safi kabisa;

22 makasi na mabeseni, sahani za kuwekea ubani na vyetezo vya kubebea moto, vyote vya zahabu safi, pete za hekalu za milango ya Pahali Patakatifu Sana, na za milango mingine ya vyumba vya ndani, zote zilitengenezwa na zahabu.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan