Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

1 Yoane 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Watoto wa Mungu

1 Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.

2 Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.

3 Basi, kila mutu anayekuwa na tumaini hili katika Kristo anajisafisha mwenyewe kama vile Kristo anavyokuwa safi.

4 Kila mutu anayefanya zambi anavunja sheria ya Mungu, kwa sababu kufanya zambi ni kuvunja sheria.

5 Ninyi munajua kwamba Yesu Kristo alikuja kusudi aondoe zambi, na hakuna zambi ndani yake.

6 Basi kila mutu anayeungana naye hafanyi tena zambi; lakini kila mutu anayefanya zambi hakumwona wala kumujua.

7 Watoto wangu, mutu asiwadanganye! Mutu anayetenda mambo ya haki ni mwenye haki kama vile Kristo ni mwenye haki.

8 Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.

9 Kila mutu anayekuwa mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa sababu neno la Mungu linakaa ndani yake; tena hawezi kufanya zambi, maana Mungu ni baba yake.

10 Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Kupendana

11 Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.

12 Tusikuwe kama Kaina aliyekuwa wa yule Mwovu, akamwua ndugu yake. Yeye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.

13 Basi wandugu zangu, musishangae kama watu wa dunia hii wakiwachukia ninyi.

14 Sisi tunajua kwamba tumeponyoka lufu na kupata uzima kwa sababu tunawapenda wandugu zetu. Mutu asiyekuwa na upendo ni kama mufu.

15 Kila mutu anayemuchukia ndugu yake ni mwuaji, nanyi munajua kwamba mwuaji yeyote hana uzima wa milele ndani yake.

16 Sisi tumetambua upendo kwa njia hii: Yesu Kristo alitoa uzima wake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kutoa uzima wetu kwa ajili ya wandugu zetu.

17 Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?

18 Watoto wangu, upendo wetu usikuwe wa masemi tu; lakini unapaswa kuwa upendo wa kweli na unaoonekana kwa matendo.


Tumaini kwa Mungu

19 Kwa njia hii tutatambua kwamba sisi ni watu wa ukweli, na mioyo yetu itatulia mbele ya Mungu.

20 Kwa maana hata kama zamiri yetu inatuhukumu, tunajua kwamba mafikiri ya Mungu yanapita zamiri yetu, naye anajua yote.

21 Wapendwa wangu, zamiri yetu isipotuhukumu, sisi tuko na tumaini mbele ya Mungu.

22 Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.

23 Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.

24 Mutu anayetii amri za Mungu anakaa ndani yake, na Mungu anakaa ndani ya yule mutu. Tunatambua kwamba Mungu anakaa ndani yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan