1 Wafalme 8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sanduku la Agano linaletwa ndani ya hekalu ( 2 Sik 5.2–6.2 ) 1 Basi, mufalme Solomono akawakusanya mbele yake kule Yerusalema wazee na viongozi wote wa makabila na wa ukoo za Waisraeli kusudi waliondoe Sanduku la Agano la Yawe katika muji wa Daudi, ni kusema Sayuni. 2 Halafu watu hao wote wakakusanyika mbele ya mufalme Solomono wakati wa sikukuu ya mwezi wa Etanimu, ni kusema mwezi wa saba. 3 Kisha kufika kwa wazee wote wa Israeli, makuhani walibeba Sanduku la Agano. 4 Walawi na makuhani walihamisha Sanduku la Agano na hema la mukutano, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwa mule ndani ya hema. 5 Mufalme Solomono na mukutano wote wa Israeli wakakusanyika mbele ya Sanduku la Agano, nao wakatoa sadaka: ngombe na kondoo wasiohesabika. 6 Kisha makuhani wakaliingiza Sanduku la Agano la Yawe kwa nafasi yake katika chumba cha ndani cha nyumba, ni kusema Pahali Patakatifu Sana, chini ya mabawa ya makerubi. 7 Hao makerubi walitandaza mabawa yao juu ya pahali Sanduku lilipowekwa, juu ya Sanduku ile na miti yake ya kulibebea. 8 Kwa sababu miti hiyo ilikuwa mirefu sana, incha zake ziliweza kuonekana kutoka Pahali Patakatifu, mbele ya chumba cha ndani; lakini haikuweza kuonekana kutoka upande wa inje. Miti hiyo ingali pahali pale hata leo. 9 Hakukukuwa kitu ndani ya Sanduku la Agano lakini vile vibao viwili vya mawe ambavyo Musa aliviweka mule kule Horebu, pahali Yawe alipofanya agano na Waisraeli walipotoka katika inchi ya Misri. 10 Makuhani walipotoka pale Pahali Patakatifu, wingu liliijaza nyumba ya Yawe. 11 Nao makuhani walishindwa kutumika ndani kwa sababu ya wingu hilo; kwa sababu utukufu wa Yawe uliijaza nyumba ya Yawe. 12 Halafu Solomono akasema: “Yawe alisema kwamba atakaa katika giza nene. 13 Hakika, nimekujengea nyumba ya kukaa, pahali pa makao yako ya milele.” Hotuba ya Solomono ( 2 Sik 6.12-42 ) 14 Kisha, Solomono akawaelekea Waisraeli wote walipokuwa wakisimama, akawabariki, 15 akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu yake ametimiza ahadi yake aliyomupa baba yangu Daudi, akisema: 16 ‘Tangu nilipowaondoa watu wangu Waisraeli katika inchi ya Misri, sikuchagua muji wowote katika makabila ya Waisraeli kusudi nijengewe nyumba nitakamoabudiwa; lakini nilimuchagua Daudi, atawale watu wangu, Waisraeli.’ 17 Kwa hiyo, baba yangu alikusudia kumujengea Yawe, Mungu wa Israeli nyumba. 18 Lakini Yawe alimwambia baba yangu Daudi: ‘Ni vizuri kwamba ulikusudia ndani ya moyo wako kunijengea nyumba. 19 Hata hivyo, si wewe utakayenijengea nyumba, lakini ni mwana wako utakayemuzaa ndiye atakayenijengea hiyo nyumba.’ 20 Na sasa, Yawe ametimiza ahadi yake, maana nimekuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, na kukiikalia kiti cha kifalme cha Israeli kama vile Yawe alivyoahidi. Tena nimejenga nyumba ya kumwabudia Yawe, Mungu wa Israeli. 21 Zaidi ya hayo, nimetenga nafasi ya kuweka Sanduku la Agano ambalo ndani yake muko agano Yawe alilofanya na babu zetu, wakati alipowatoa katika inchi ya Misri.” 22 Kisha Solomono alisimama kwenye mazabahu ya Yawe, mbele ya Waisraeli wote, aliinua mikono yake juu, 23 akasema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, juu mbinguni, au chini katika dunia. Wewe unashika agano lako na kutenda wema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote. 24 Umetimiza ahadi uliyoitoa kwa mutumishi wako Daudi baba yangu; hakika, yale uliyosema umeyatimiza leo kwa uwezo wako mwenyewe. 25 Kwa hiyo, sasa, ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba vilevile utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu mumoja wa uzao wako kwa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako watakuwa waangalifu juu ya mwenendo wao mbele yangu kama wewe ulivyofanya mbele yangu.’ 26 Basi, ee Mungu wa Israeli, ninakusihi utimize hayo yote uliyomwahidi mutumishi wako Daudi, baba yangu. 27 “Lakini, ee Mungu, kweli utakaa katika dunia? Ikiwa hata mbingu zenyewe wala mbingu za juu sana hazikutosha, namna gani nyumba hii ambayo nimeijenga itakutoshelea? 28 Hata hivyo, ee Yawe, Mungu wangu, unigeukie mimi mutumishi wako ninapokuomba na kukusihi. Usikilize malalamiko na maombi ambayo mimi mutumishi wako ninaomba leo. 29 Uchunge nyumba hii usiku na muchana, nafasi ambapo umesema: ‘Hapo ndipo watu watakapoliheshimu jina langu’. Unisikilize ninapokuja pahali hapa kwa kuomba. 30 Usikilize wakati tunapokusihi, mimi mutumishi wako na watu wako Waisraeli ambao tutaomba tukielekea pahali hapa. Kutokea kwako mbinguni, usikilize. Na ukisha kusikiliza, utusamehe. 31 “Mutu akimukosea mwenzake, naye akiletwa apate kuapa mbele ya mazabahu yako katika nyumba hii, naye akiapa, 32 tafazali wewe usikilize kutokea kule mbinguni, utende na kuwahukumu watumishi wako. Anayekuwa na kosa umwazibu kwa kadiri ya makosa yake; asiyekuwa na kosa umwachilie na kumupatia haki kwa kadiri ya haki yake. 33 “Ikiwa watu wako Waisraeli wameshindwa na waadui zao kwa sababu ya zambi walizotenda mbele yako, nao wakikugeukia na kusifu jina lako, wakiomba na kukusihi katika nyumba hii, 34 basi, uwasikilize kutokea kule mbinguni, uwasamehe watu wako Waisraeli zambi zao, halafu uwarudishe katika inchi uliyowapa babu zao. 35 “Mvua isiponyesha kwa sababu wametenda zambi mbele yako na unawaazibu, wakiomba wakielekea pahali hapa na kusifu jina lako, vilevile wakiziacha zambi zao na kukurudilia, 36 tafazali, uwasikilize kutokea kule mbinguni, usamehe zambi za watumishi wako, watu wako Waisraeli, na uwafundishe kufuata njia nzuri. Kisha unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako kwamba itakuwa mali yao. 37 “Ikiwa kuna njaa katika inchi, au ugonjwa mukali, ukosefu wa mvua, ugonjwa wa mimea, nzige au vidudu vingine, au ikiwa watu wako wameshambuliwa na waadui zao katika muji wao wowote, ikiwa kuna pigo lolote au ugonjwa wowote, 38 tafazali, chochote ambacho mutu yeyote au watu wako wote wa Waisraeli wanakuomba na kukusihi, kila mutu akijua taabu ndani ya moyo wake na kunyoosha mikono yake kuelekea nyumba hii, 39 basi, usikilize kule kwako mbinguni, uwasamehe na kumutendea kila mutu kwa kadiri anavyostahili, maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote, 40 kusudi wakutii wakati wote wanapoishi katika inchi uliyowapa babu zetu. 41 “Hata wakati mugeni asiyekuwa mumoja wa watu wako Waisraeli akikuja kutoka inchi ya mbali kwa ajili ya jina lako, 42 maana watu wa mataifa mengine watasikia sifa zako na juu ya nguvu na uwezo wako, mutu yule akikuja na kuomba akielekea nyumba hii, 43 usikilize kutokea kwako mbinguni. Umujalie yule mugeni yote atakayokulilia, kusudi watu wote katika ulimwengu wapate kujua jina lako na kukutii kama watu wako Waisraeli wanavyofanya, na wapate kufahamu kwamba nyumba hii ambayo nimeijenga, inajulikana kwa jina lako. 44 “Watu wako wakienda kwa vita kupigana na adui yao kwa upande wowote utakapowapeleka, nao wakikuomba wakielekea muji uliouchagua na nyumba niliyoijenga kwa ajili ya jina lako, 45 usikilize kutoka mbinguni wanapokuomba na kukusihi. Uwapatie ushindi katika vita. 46 “Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, nawe ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na adui, hata wapelekwe mateka mpaka katika inchi ya adui inayokuwa mbali au karibu, 47 kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’, 48 vilevile wakati ule watakapokuwa katika inchi ya waadui zao, wakikugeukia kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote, na kama wakikuomba wakielekea inchi yao ambayo uliwapatia babu zao, wakielekea muji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako, 49 basi, kutoka kwako mbinguni usikilize wakati wanakuomba na kukusihi. Uwasaidie. 50 Uwasamehe watu wako zambi walizotenda mbele yako na uasi wao, uwahurumie mbele ya waadui zao, kusudi nao wapate kuwahurumia, 51 maana ni watu wako, na ni mali yako, watu ambao uliwatoa Misri kutoka katika furu ya chuma. 52 “Uangalie wakati mutumishi wako anapokusihi na wakati watu wako Waisraeli wanapokusihi. Uwasikilize kila mara wanapokulilia. 53 Kwa sababu, ee Bwana wetu Yawe, uliwatenga na watu wa mataifa mengine katika dunia, kusudi wakuwe mali yako, kama ulivyotangaza kwa njia ya Musa, mutumishi wako, wakati ule ulipowatoa babu zetu katika inchi ya Misri.” Ombi la mwisho 54 Solomono alipomaliza kusema maombi hayo yote na ombi lake kwa Yawe, alisimama kutoka pale mbele ya mazabahu ya Yawe, pahali alipokuwa amepiga magoti akiinua mikono yake juu. 55 Alisimama, akawabariki Waisraeli wote waliokuwa wamekusanyika pale, akisema kwa sauti kubwa: 56 “Atukuzwe Yawe ambaye amewapatia watu wake Waisraeli amani, kulingana na ahadi yake. Ametimiza ahadi zake zote njema alizozitoa kupitia kwa mutumishi wake Musa. 57 Yawe, Mungu wetu, akuwe nasi kama alivyokuwa na babu zetu. Tunaomba asituachilie, wala asitutupilie. 58 Yeye aelekeze mioyo yetu kwake, kusudi tufuate njia zake, tukishika amri zake, masharti yake na maagizo yake aliyowapa babu zetu. 59 Basi, maneno yangu haya ambayo ni ombi langu mbele ya Yawe, yakuwe karibu na Yawe, Mungu wetu, muchana na usiku, naye amujalie mutumishi wake, na watu wake Waisraeli, kusudi wafanikiwe katika mahitaji yao ya kila siku. 60 Nayo mataifa yote katika ulimwengu yatajua kwamba kweli Yawe ndiye Mungu wala hakuna mwingine. 61 Nanyi, mukuwe waaminifu kwa Yawe, Mungu wetu, mukifuata masharti yake na kutii amri zake zote kama munavyofanya hivi leo.” Hekalu linazinduliwa ( 2 Sik 7.4-10 ) 62 Kisha, mufalme Solomono na Waisraeli wote waliokuwa pamoja naye walimutolea Yawe sadaka. 63 Naye Solomono alimutolea Yawe sadaka za amani: ngombe elfu makumi mbili na mbili na kondoo elfu mia moja na makumi mbili. Hivi ndivyo mufalme na watu wote wa Israeli walivyozindua nyumba ya Yawe. 64 Siku hiyohiyo, mufalme aliizindua sehemu ya katikati ya uwanja uliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe, maana ni pale ndipo alipotolea sadaka za kuteketezwa, sadaka za ngano, na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu ile mazabahu ya shaba haikutosha kwa sadaka hizo zote. 65 Naye Solomono kwa muda wa siku saba alifanya sikukuu pamoja na Waisraeli wote. Nao walitoka tangu kwenye kiingilio cha Hamati, mpaka muto wa Misri. 66 Katika siku ya nane, Solomono aliwaaga watu; nao wakamutakia mufalme baraka, wakaenda kwao wakishangilia na kufurahi kwa sababu ya wema ambao Yawe aliuonyesha kwa Daudi, mutumishi wake, na kwa watu wake Waisraeli. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo