Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

1 Wafalme 19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Elia juu ya mulima Horebu

1 Mufalme Ahabu alimwelezea muke wake Yezebeli mambo yote Elia aliyofanya na jinsi alivyowaua manabii wa Bali kwa upanga.

2 Yezebeli akatuma mujumbe kwa Elia amwambie: “Miungu waniue, ninakuapia, kama kesho nisipokuua kwa wakati kama huu sawa vile ulivyowaua wale manabii.”

3 Elia akakimbilia katika muji wa Beri-Seba katika jimbo la Yuda, kule alikomwacha mutumishi wake,

4 naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”

5 Basi, Elia akalala chini ya muti ule, akashikwa na usingizi. Kisha muda kidogo, malaika akakuja, akamugusa na kumwambia: “Amuka ukule.”

6 Elia alipoangalia, akaona mukate uliokaangwa juu ya makaa, na chupa ya maji karibu na kichwa chake. Basi, akakula, akakunywa na akalala tena.

7 Malaika wa Yawe akamufikia tena kwa mara ya pili, akamugusa na kumwambia: “Amuka ukule, kama sivyo safari itakuwa ngumu sana kwako.”

8 Elia akaamuka, akakula na kunywa. Kisha akatembea kwa nguvu ya chakula hicho mwendo wa siku makumi ine, muchana na usiku, mpaka Horebu kwenye mulima wa Mungu.

9 Kule, akafika kwenye pango, akakaa mule. Mara moja Yawe akamutolea ujumbe: “Elia! Unafanya nini hapa?”

10 Naye akasema: “Ninaona uchungu na wivu, ee Yawe, Mungu wa majeshi, kwa sababu watu wa Israeli wamevunja agano lako, wakazibomoa mazabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga; ni mimi tu niliyebaki, nami vilevile wananiwinda waniue!”

11 Yawe akamwambia: “Kwenda usimame juu ya mulima, mbele yangu mimi Yawe.” Basi, Yawe akapita na kuuvumisha upepo mukali ambao uliporomosha milima na kuvunja mawe makubwa. Lakini Yawe hakukuwa katika upepo ule. Upepo ukapita, kukakuwa tetemeko la inchi. Lakini Yawe hakukuwa katika tetemeko la inchi.

12 Tetemeko likapita, kukakuwa moto. Lakini Yawe hakukuwa katika moto ule. Nyuma ya moto, kukatokea sauti ndogo, tulivu.

13 Basi, Elia aliposikia sauti hiyo, alijifunika uso kwa koti lake, akatoka na kusimama kwenye mulango wa pango. Halafu, akasikia sauti: “Elia! Unafanya nini hapa?”

14 Naye akasema: “Ninaona uchungu na wivu, ee Yawe, Mungu wa majeshi, kwa sababu watu wa Israeli wamevunja agano lako, wakazibomoa mazabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga; ni mimi tu niliyebaki, nami vilevile wananiwinda waniue!”

15 Yawe akamwambia: “Urudie kwa kupitia njia ya jangwa mpaka Damasiki. Utakapofika, umupakae Hazaeli mafuta akuwe mufalme wa Aramu.

16 Naye Yehu mwana wa Nimusi, umupakae mafuta akuwe mufalme wa Israeli. Elisha mwana wa Safati wa Abeli-Mehola, utamupakaa mafuta akuwe nabii kwa pahali pako.

17 Basi, mutu yeyote atakayepona kuuawa kwa upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua, na yeyote atakayepona kuuawa kwa upanga wa Yehu, Elisha atamwua.

18 Lakini, nitawaacha wazima watu elfu saba katika inchi ya Israeli, ambao hawajainama mbele ya Bali, wala kuibusu sanamu yake.”


Elisha anaitwa kuwa nabii

19 Elia akaondoka, akamukuta Elisha mwana wa Safati akilima. Pale, kulikuwa makundi kumi na mbili ya ngombe dume wawiliwawili wakilima, na ngombe wawili wa Elisha walikuwa wa nyuma kabisa. Basi, Elia akavua koti lake na kumutupia.

20 Halafu, Elisha akawaacha ngombe wake, akamufuata Elia mbio na kumwambia: “Uniruhusu kwanza niende kumupa baba yangu na mama yangu busu la kwa heri, kisha nikufuate.” Elia akamujibu: “Kwenda! Ni nini niliyokutendea?”

21 Basi, Elisha akamwacha Elia, akarudilia ngombe wake, akawachinja ngombe hao na kuwapika akitumia miti ya nira kama kuni, akawapa watu, wakakula. Kisha akaondoka, akamufuata Elia na kuwa mutumishi wake.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan