1 Samweli 12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Samweli anawahutubia Waisraeli 1 Samweli akawaambia Waisraeli wote: “Maneno yote muliyoniambia, nimeyasikiliza. Nimemusimika mufalme juu yenu. 2 Sasa, munakuwa na mufalme wa kuwaongoza. Kwa upande wangu, mimi ni muzee mwenye imvi, na wana wangu wako pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu nilipokuwa kijana mpaka sasa. 3 Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.” 4 Watu wakamujibu: “Haujatudanganya hata kidogo, haujatugandamiza, wala haujakamata kitu chochote kwa mutu.” 5 Samweli akajibu: “Yawe ni mushuhuda juu yenu, na mufalme wake muchaguliwa leo ni mushuhuda kuwa mumeniona sina kosa.” Wao wakajibu: “Yeye ni mushuhuda.” 6 Samweli akawaambia: “Yawe ndiye aliyemuchagua Musa na Haruni na kuwaondoa babu zenu katika inchi ya Misri. 7 Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu. 8 “Yakobo na jamaa yake walipokwenda Misri, na Wamisri walipowagandamiza, babu zenu walimulilia Yawe. Naye akawatuma Musa na Haruni ambao waliwatoa babu zenu katika inchi ya Misri na kuwafanya mukae katika inchi hii. 9 Lakini wao walimusahau Yawe, Mungu wao, naye akawatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa waaskari wa muji wa Hazori, na katika mikono ya Wafilistini na katika mikono ya mufalme wa Moabu. Mataifa hayo yalipigana na babu zenu na kuwashinda. 10 Babu zenu wakamulilia Yawe, wakisema: ‘Tumefanya zambi kwa sababu tumekuacha wewe Yawe, kwa kutumikia sanamu za mungu Bali na Astaroti. Utuokoe kutoka katika mikono ya waadui zetu, nasi tutakutumikia’. 11 Halafu Yawe alimutuma Yerubali, na kisha akamutuma Bedani, kisha Yefuta, na kwa mwisho akanituma mimi Samweli. Kila mumoja wetu aliwaokoa kutoka waadui zenu waliowazunguka, nanyi mukaishi kwa amani. 12 Lakini mulipomwona mufalme Nahasi wa Waamoni amekuja kuwashambulia, mukamukataa Yawe ambaye ndiye Mufalme wenu, mukaniambia: ‘Hapana! Mufalme ndiye atakayetutawala’. 13 Sasa, mufalme muliyejichagulia ndiye huyu hapa. Mulimwomba Yawe awape mufalme, naye amewapa. 14 Kama mukimutii Yawe na kumutumikia na kusikiliza sauti yake bila kuiasi amri yake, kama ninyi wenyewe pamoja na mufalme anayewatawala mukimufuata Yawe, Mungu wenu, basi mutafanikiwa. 15 Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu. 16 Kwa hiyo basi, mutulie na kulitazama jambo hilo kubwa ambalo Yawe atatenda mbele yenu. 17 Sasa si wakati wa kuvuna ngano? Lakini mimi nitamwomba Yawe alete radi na mvua, nanyi mutatambua na kuona kwamba uovu wenu muliotenda mbele ya Yawe kwa kujitakia mufalme, ni mukubwa.” 18 Basi, Samweli akamwomba Yawe, naye akatuma radi na mvua katika siku hiyo. Watu wote wakamwogopa sana Yawe na Samweli. 19 Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.” 20 Samweli akawajibu: “Musiogope. Ingawa mumefanya uovu huu, musiache kumufuata Yawe, lakini mumutumikie kwa moyo wenu wote. 21 Musiifuate miungu ya uongo isiyokuwa na faida wala haiwezi kuwaokoa, maana ni ya uongo. 22 Kwa heshima ya jina lake kubwa, Yawe hatawatupa watu wake kwa sababu amependa kuwafanya ninyi mukuwe watu wake. 23 Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki. 24 Basi, ninyi mumutii Yawe na kumutumikia kwa uaminifu, kwa moyo wenu wote. Mukumbuke yale mambo makubwa aliyowatendea. 25 Lakini kama mukiendelea kutenda maovu, mutaangamia ninyi wenyewe pamoja na mufalme wenu.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo