1 Mambo ya Siku 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Wana wa mufalme Daudi 1-3 Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa wakati alipokuwa kule Hebroni: Amunoni, muzaliwa wake wa kwanza. Mama yake aliitwa Ahinoamu, wa muji wa Yezereheli; wa pili: Danieli ambaye mama yake aliitwa Abigaili wa muji wa Karmeli; wa tatu: Abusaloma, ambaye mama yake aliitwa Maka, binti ya Talmai mufalme wa Gesuri; wa ine: Adonia, ambaye mama yake aliitwa Hagiti; wa tano: Sefatia, ambaye mama yake aliitwa Abitali; wa sita: Itiramu, ambaye mama yake aliitwa Egla. 4 Wote sita, walizaliwa Hebroni ambako Daudi alitawala kwa muda wa miaka saba na nusu. Kule Yerusalema, alitawala kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu. 5 Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa alipokuwa Yerusalema: Muke wake Bati-Seba, binti ya Amieli, akamuzalia wana wane: Simea, Sobabu, Natani na Solomono. 6 Na zaidi ya hao alikuwa na wana wengine tisa: Ibuhari, Elisua, Elifeleti, 7 Noga, Nefegi, Yafia, 8 Elisama, Eliada na Elifeleti. 9 Hao wote walikuwa wana wa Daudi, zaidi ya wale kuna wengine aliozaliwa na wahabara yake. Daudi alikuwa na binti vilevile, aliyeitwa Tamari. 10-14 Mwana wa Solomono: Rehoboamu, mwana wa Rehoboamu: Abiya, mwana wa Abiya: Asa, mwana wa Asa: Yosafati, mwana wa Yosafati: Yoramu, mwana wa Yoramu: Ahazia, mwana wa Ahazia: Yoasi, mwana wa Yoasi: Amazia, mwana wa Amazia: Azaria, mwana wa Azaria: Yotamu, mwana wa Yotamu: Ahazi, mwana wa Ahazi: Hezekia, mwana wa Hezekia: Manase, mwana wa Manase: Amoni, mwana wa Amoni: Yosia. 15 Wana wa Yosia walikuwa: Yohana, muzaliwa wake wa kwanza; wa pili Yoyakimu, wa tatu Zedekia na wa ine Salumu. 16 Wana wa Yoyakimu walikuwa: Yekonia na Zedekia. 17 Wana wa Yekonia, aliyepelekwa kuwa mufungwa na Wababeli, walikuwa: Saltieli, 18 Malkiramu, Pedaya, Senazari, Yekamia, Hosama na Nedabia. 19 Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Simei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Mesulamu na Hanania. Alikuwa na binti mumoja, jina lake Selomiti. 20 Zerubabeli vilevile alikuwa na wana wengine watano: Hasuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yusabu-Hesedi. 21 Wana wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yesaya. Mwana wa Yesaya: Refaya. Mwana wake: Arnani. Mwana wake: Obadia. Mwana wake: Sekania. 22 Mwana wa Sekania: Semaya. Wana wa Semaya walikuwa sita: Hatusi, Igali, Baria, Nearia na Safati. 23 Nearia alikuwa na wana watatu: Eliyoenai, Hezekia na Azirikamu. 24 Eliyoenai alikuwa na wana saba: Hodavia, Eliasibu, Pelaya, Akubu, Yohana, Dalaya na Anani. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo