Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.
kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’
Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.
Kwa maana hamukupewa roho anayewafanya muishi katika utumwa na kuwatia tena woga, lakini mulipewa Roho anayewafanya mukubaliwe kuwa watoto wa Mungu. Na kwa uwezo wa Roho huyo, tunaweza kumwita Mungu “Baba.”
Wandugu zangu, niseme nini basi? Wakati munapokusanyika kwa ibada, mumoja anaweza kuimba wimbo, mwingine kufundisha, mwingine kutoa ufunuo, mwingine kusema kwa luga za ajabu na mwingine anaweza kutafsiri. Na hayo yote yanapaswa kufanyika katika nia ya kujenga kanisa katika imani.
Kwa uongozi wake, viungo vyote vya mwili vinashikamana kabisa, nao mwili wote muzima unashikamana vizuri kwa nguvu ya maunganio yake. Halafu, kila kiungo kinapotumika kama kinavyopaswa, mwili wote unakomaa na kujijenga katika upendo.
Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.
Mukuwe na mizizi ndani yake, mujijenge juu yake na kusimama imara katika imani sawa vile mulivyofundishwa. Na zaidi ya hii mukuwe wenye kushukuru sana.
Uwaambie wasishikamane na hadisi za uongo, pamoja na mambo yasiyokuwa na mwisho ya wababu. Hayo yote yanaleta mabishano, wala hayafai kitu kwa kutimiza mupango wa Mungu wa wokovu, unaojulikana kwa njia ya imani.
Ninakumbuka vilevile imani yako isiyokuwa ya udanganyifu, imani ile tate muzaa mama yako Loisi na mama yako Euniki waliyokuwa nayo. Ninajua hakika kwamba wewe vilevile uko nayo.
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Mungu na mutume wa Yesu Kristo. Mimi nimetumwa kwa kuongoza watu waliochaguliwa na Mungu wapate kumwamini na kutambua ukweli unaolingana na dini yetu.
Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.
Wapendwa wangu, wakati nilipokuwa nikifanya bidii sana ya kuwaandikia juu ya wokovu tunaoshiriki wote pamoja, nikaona sherti niwaandikie na kuwaonya mupate kutetea imani ile Mungu aliyotoa mara moja tu kwa watu wake.
Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”