Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 6:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Lakini yule kahaba Rahabu pamoja na watu wote wa nyumba ya baba yake, Yoshua akayaokoa maisha yao. Rahabu akaishi kati ya Waisraeli mpaka leo, kwa sababu aliwaficha wajumbe ambao Yoshua aliwatuma kwenda kuupeleleza muji wa Yeriko.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 6:25
11 Σταυροειδείς Αναφορές  

Halafu watu wote watakaoomba kwa jina la Bwana ataokolewa.’


Kwa njia ya imani, Rahaba, yule kahaba, hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wapelelezi kwa amani.


Ilikuwa hivi vilevile kwa yule kahaba Rahaba. Mungu alimuhesabia haki kwa njia ya matendo yake, wakati alipowakaribisha wapelelezi na kuwatorosha kwa njia nyingine.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.


Tutakapokuja katika inchi hii, funga kamba hii nyekundu kwenye dirisha ambalo umetuteremushia. Uwakusanye hapa kwako baba yako, mama yako na kaka zako na jamaa yote ya baba yako.


Lakini, yule mwanamuke alikuwa amekwisha kuwaficha watu hao wawili. Basi, akawaambia wajumbe hao: “Ni kweli kwamba hao watu walikuja kwangu, lakini mimi sikujua wametoka wapi.


Lakini Rahabu alikuwa amewapandisha hao wapelelezi juu ya dari na kuwaficha kwa vijiti vya kitani alivyokuwa ametandaza juu ya dari.


Yoshua akasimika vilevile mawe kumi na mawili katikati ya muto Yordani, pahali pale miguu ya makuhani waliobeba lile Sanduku la Agano iliposimama. Mawe hayo yako kule mpaka hivi leo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις