Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 6:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Kisha wakaangamiza kila kitu katika muji ule na kuwaua kwa upanga: wanaume na wanawake, vijana na wazee, ngombe, kondoo na punda.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 6:21
20 Σταυροειδείς Αναφορές  

Basi, nabii akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Umemwachilia akuponyoke mutu ambaye niliamuru auawe. Basi, maisha yake utalipa kwa maisha yako, na watu wake kwa watu wako.’ ”


Enyi wenyeji wa Diboni: mushuke kutoka pahali penu pa utukufu, muikae juu ya udongo usiokuwa na maji. Maana mwangamizaji wa Moabu, amefika kuwashambulia; amekwisha haribu kuta zenu.


hakika mutawaua kwa upanga watu wa muji huo. Mutauteketeza kwa upanga kabisa na ngombe wote vilevile.


Tukaiteka na kuiharibu miji yake yote, tukaua wanaume na wanawake na watoto. Hatukumwacha mutu yeyote muzima.


Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.


Siku hiyo Yoshua alipouteka muji wa Makeda, alimuua mufalme wake na wakaaji wake wote bila kuacha hata mutu mumoja. Alimutendea mufalme wa Makeda kama vile alivyomutendea mufalme wa Yeriko.


Waliuteka muji huo na mufalme wake pamoja na miji mingine yote iliyouzunguka na kuwaangamiza wote waliokuwa ndani yao bila kuacha hata mutu mumoja. Waliutendea muji huo kama walivyoutendea muji wa Hebroni na muji wa Libuna na wafalme wao.


Kisha akauteketeza muji wa Hazori kwa moto na kuwaua wakaaji wake wote, hakumwacha hata mutu mumoja.


Waisraeli wakatwaa vitu vyote walivyonyanganya na nyama wa miji hiyo; lakini waliwaua wakaaji wake wote, wala hawakumwacha hata mutu mumoja.


Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”


Watu waliobaki katika muji walitoka, lakini wote wakakuwa wamezungukwa na Waisraeli; nao wakauawa, wala hakukubaki hata mumoja wao.


Lakini wakaaji wa Gibeoni walipopata habari juu ya jinsi Yoshua alivyoitendea miji ya Yeriko na Ai,


Kisha malaika mumoja mwenye uwezo akanyanyua jiwe linalokuwa kama jiwe kubwa la kusagia. Akalitupa katika bahari akisema: “Ni hivi muji mukubwa wa Babeli utakavyotupwa kwa nguvu, nao hautaonekana tena.


Sasa, uende kushambulia na kuangamiza vitu vyote wanavyokuwa navyo. Usiwaache wazima, lakini uwaue wote: wanaume kwa wanawake, watoto wachanga na wenye kunyonya, ngombe, kondoo, ngamia na punda.’ ”


Alimukamata mateka mufalme Agagi wa Waamaleki akiwa angali muzima. Akawaua watu kwa makali ya upanga.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις