Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 6:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Muji ule utaangamizwa na kila kitu kinachokuwa mule maana umetolewa kwa Yawe. Rahabu, yule kahaba, ndiye atakayeachwa pamoja na wale ambao wako ndani ya nyumba yake kwa sababu aliwaficha wapelelezi wetu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 6:17
26 Σταυροειδείς Αναφορές  

Anayekubariki, nitamubariki, anayekulaani, nitamulaani. Kwa njia yako, nitabariki mataifa yote ya dunia.”


Ikiwa mutu yeyote atashindwa kufika katika muda wa siku tatu, kulingana na amri iliyotolewa na viongozi, mali yake yote itanyanganywa, naye mwenyewe atatengwa mbali na makutano na jamii ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho.


Upanga utajaa damu na mafuta: damu ya kondoo na mbuzi, na mafuta ya figo za kondoo dume. Maana Yawe ana sadaka huko Bosira, kutakuwa mauaji makubwa katika inchi ya Edomu.


Lakini siku hiyo ni siku ya Bwana wetu Yawe wa majeshi. Ni siku ya kulipiza kisasi, siku ya kuwaazibu waadui zake. Upanga utawamaliza hao na kutosheka, utaikunywa damu yao na kushiba. Maana Bwana wetu Yawe wa majeshi yuko na sadaka huko kaskazini karibu na muto Furati.


Sasa, ewe mwanadamu, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Uite ndege wote na nyama wote wa pori wakusanyike toka pande zote na kuja kukula karamu ya sadaka ya nyama ninayowatayarishia, ambayo itakuwa kubwa sana juu ya milima ya Israeli, ambako watakula nyama na kunywa damu.


Katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano shamba hilo litaachiliwa na kuwa la Yawe milele. Kuhani ndiye atakayelirizi.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


Ninatangaza hekima ya siri ya Mungu, hekima iliyofichwa kwa watu, na iliyopangwa na Mungu mbele ya kuumbwa kwa dunia kwa ajili ya utukufu wetu.


Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”


Na tena hakuna ushirika kati ya Sheria na imani. Lakini Maandiko Matakatifu yanasema: “Yule anayeshika maagizo ya Sheria hii ataishi kwa njia hiyo.”


Mutawaangamiza watu wote: Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi kama vile Yawe, Mungu wenu alivyoamuru,


Kwa njia ya imani, Rahaba, yule kahaba, hakuangamia pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa sababu aliwakaribisha wapelelezi kwa amani.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Ilikuwa hivi vilevile kwa yule kahaba Rahaba. Mungu alimuhesabia haki kwa njia ya matendo yake, wakati alipowakaribisha wapelelezi na kuwatorosha kwa njia nyingine.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.


Wapelelezi hao waliondoka wakaenda kwenye milima. Walikaa kule kwa muda wa siku tatu mpaka wale waliokuwa wanawafuatilia waliporudi katika muji Yeriko, nyuma ya kuwatafuta na kukosa kuwaona.


Lakini Waisraeli hawakukuwa waaminifu juu ya vile vitu vilivyotolewa viangamizwe maana Akana mwana wa Karmi, mujukuu wa Zabedi, wa ukoo wa Zera, wa kabila la Yuda, alitwaa vimoja kati ya vitu vilivyoamriwa viteketezwe. Kwa hiyo hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli.


Sasa, uende kushambulia na kuangamiza vitu vyote wanavyokuwa navyo. Usiwaache wazima, lakini uwaue wote: wanaume kwa wanawake, watoto wachanga na wenye kunyonya, ngombe, kondoo, ngamia na punda.’ ”


Saulo akawaambia Wakeni: “Muende! Muondoke! Mutoke kati ya Waamaleki, kama sivyo, nitawaangamiza pamoja nao. Muondoke kwa sababu ninyi muliwatendea mema Waisraeli walipotoka Misri.” Basi, Wakeni wakaondoka kati ya Waamaleki.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις