Enyi watu wangu, mukumbuke mipango mibaya ya Balaki mufalme wa Moabu, na jinsi Balama mwana wa Beori alivyomujibu. Mukumbuke yaliyotukia katika njia kati ya Sitimu na Gilgali. Mukumbuke, mutambue matendo yangu ya kuwaokoa!
Kisha Waisraeli wakatuma wajumbe kwa mufalme wa Edomu wakimwomba awaruhusu kupita katika inchi yake, lakini mufalme wa Edomu akakataa. Basi wakamwomba mufalme wa Moabu ruhusa naye vilevile akakataa. Kwa hiyo Waisraeli wakabaki Kadesi.