Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 24:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yoshua akawaambia watu wote: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Hapo zamani, wazee wenu waliishi ngambo ya muto Furati, wakaitumikia miungu mingine. Muzee mumoja aliitwa Tera, baba ya Abrahamu na Nahori.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 24:2
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Serugi alipokuwa na umri wa miaka makumi tatu, akazaa Nahori.


Nahori alipokuwa na umri wa miaka makumi mbili na tisa, akazaa Tera.


Tera alipokuwa na umri wa miaka makumi saba, akazaa Abramu, Nahori, na Harani.


Hawa ndio wazao wa Tera, baba ya Abramu, Nahori na Harani. Harani alikuwa baba ya Loti.


Wakati ule Labani alikuwa amekwenda kukata manyoya ya nyama wake. Hivyo Rakeli akapata nafasi ya kuiba sanamu za miungu ya baba yake.


Ninajua ulitoroka kwa sababu ya hamu kubwa ya kurudi katika nyumba ya baba yako. Lakini kwa nini uliiba sanamu za miungu yangu?”


Lakini ukipata mumoja kati yetu na sanamu za miungu yako, atakufa! Mbele ya hawa wandugu zetu, onyesha chochote kinachokuwa chako, ukitwae.” Yakobo hakujua kwamba Rakeli alikuwa ameiba sanamu za miungu ya Labani.


Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, ataamua kati yetu.” Basi, Yakobo akaapa kwa Mungu ambaye ni kitisho cha baba yake Isaka.


Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.


Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.


Uuambie kwamba Bwana wake Yawe anauambia hivi: Kwa asili wewe ulizaliwa katika inchi ya Kanana. Baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Muhiti.


utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις