Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 23:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Maana, kama mukimwasi Yawe na kujiunga na mataifa haya yaliyobaki kati yenu, mukioa kwao nao wakioa kwenu,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 23:12
28 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ndiyo maana mwanaume anamwacha baba yake na mama yake, na kuambatana na muke wake, nao wawili wanakuwa mwili mumoja.


Lakini Sekemu akavutiwa sana na yule binti, akamupenda hata akaanza kumubembeleza.


ni kusema wanawake wa mataifa ambayo Yawe alikuwa amewakataza Waisraeli akisema: “Musioe kwao wala wao wasioe kwenu kwa sababu wanawake hao watapotosha mioyo yenu kusudi muitumikie miungu yao.” Solomono aliwapenda sana wanawake hao.


Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.


Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya, uwatoweshe pamoja na watenda maovu. Amani ikuwe na Israeli!


Mwovu anajipendelea mwenyewe, anafikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Lakini, mutu wa haki akiacha haki yake na kutenda uovu na kufanya machukizo yaleyale mutu mwovu anayofanya, basi, huyo ataishi? Hapana! Matendo yake yote mema aliyotenda hayatakumbukwa tena; atakufa kwa sababu ya uasi na zambi aliyotenda.


Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Yawe, wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.


Halafu anakwenda kutwaa pepo wengine saba wanaokuwa wabaya kumupita, nao wote wanakuja kuingia na kukaa mule. Na hali ya mwisho ya mutu yule inageuka mbaya kuliko hali yake ya kwanza. Na hivi ndivyo itakavyokuwa kwa watu wa kizazi hiki kibaya.”


Basi kwa sababu ya maneno haya, wengi kati ya wanafunzi wake wakamwacha, nao hawakutembea tena pamoja naye.


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


hasira ya Yawe isiwake juu yenu, naye asiwafute katika dunia, maana Yawe, Mungu wenu, anayekuwa kati yenu, ni Mungu mwenye wivu.


Musioane nayo, wala musiyaoeshee wabinti zenu au wana wenu.


Mukifanya hivyo wao watawapotosha watoto wenu wasimufuate Yawe, na kuwafanya waabudu miungu mingine, nayo hasira ya Yawe itawaka juu yenu, halafu atawaangamiza mara moja.


Basi, mukuwe waangalifu sana kumupenda Yawe, Mungu wenu.


Mutu anayesema kwamba anaishi katika mwangaza, lakini anamuchukia ndugu yake, yeye angali anaishi katika giza.


Lakini wazazi wake wakamwambia: “Hakuna binti yeyote kati ya wandugu zako au kati ya watu wetu kusudi uende kuoa kwa Wafilistini wasiotahiriwa?” Lakini Samusoni akamwambia baba yake: “Munioee binti huyo, maana ananipendeza sana.”


Wakaoa wabinti zao na kuoesha wabinti zao kwa vijana wa mataifa hayo na kuiabudu miungu yao.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις