Akawaambia: “Mwende kwenye mulima kusudi wale wanaowafuatilia wasiwakamate. Mujifiche kule kwa muda wa siku tatu, mpaka wale wanaowafuatilia watakapokuwa wamerudi katika muji. Kisha mutaweza kujiendea.”
Basi, watu wakapiga kelele nayo mabaragumu yakiwa yanapigwa. Watu waliposikia sauti ya mabaragumu walipiga kelele kubwa, na kuta za muji zikaanguka chini kabisa. Mara tu watu wakaushambulia muji, kila mumoja kutoka pahali aliposimama, wakauteka.