Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 18:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha ulielekea chini kupitia pembeni ya mulima unaokuwa karibu na bonde la mwana wa Hinomu, ambalo lilikuwa katika sehemu ya kaskazini zaidi ya bonde la Warefaimu. Halafu mupaka uliteremuka kuelekea bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ukaendelea kuteremuka mpaka Eni-Rogeli.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 18:16
19 Σταυροειδείς Αναφορές  

Wakati ule, Yonatani na Ahimasi walikuwa wakimungojea karibu na Eni-Rogeli, kusudi wasionekane na mutu yeyote wakiingia katika muji. Kila mara mujakazi fulani alikuwa akiwapelekea habari nao wakaipeleka kwa mufalme Daudi.


Wafilistini walifika na kujitawanya kwenye Bonde la Refaimu.


Siku moja, Adonia alitoa sadaka ya kondoo, ngombe na wana-ngombe wanono kwenye Jiwe la Zoheleti, karibu na chemichemi inayoitwa Enrogeli. Akawaalika kwenye karamu ya sadaka hiyo wandugu zake wote, ni kusema wana wengine wa mufalme, na watumishi wote wa mufalme wanaokuwa wa kabila la Yuda.


Mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipoitwa Tofeti katika bonde la wana wa Hinomu, kusudi mutu yeyote asimuteketeze mwana wake au binti yake kama sadaka kwa Moleki.


Wafilistini wakafika wakaanza mashambulizi katika bonde la Refaimu.


akafukiza ubani kwenye Bonde la mwana wa Hinomu na kuwateketeza wana wake kama sadaka, akiiga desturi za kuchukiza za watu ambao walifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Na aliwatoa wana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto katika bonde la mwana wa Hinomu. Alipiga ramuli, aliaguza na alitumia hirizi; hata alishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Kweli, pahali pa kumuteketeza mufalme wa Asuria pamekwisha kutayarishwa muda murefu uliopita. Pahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Kuna moto na kuni kwa uwingi. Yawe ataupulizia pumzi yake kama kijito cha kiberiti na kuuwasha.


na kuwaambia kwamba: Yawe wa majeshi, anasema hivi: Nitavunjavunja watu hawa na muji huu sawa vile mutu anavyovunja chombo cha mufinyanzi, hata kisiweze kutengenezwa tena. Watu watazikwa Tofeti, kwa sababu hapatakuwa pahali pengine pa kuzikia.


Halafu uende pamoja nao katika bonde la Mwana wa Hinomu, kwa kupitia mulango unaoitwa mulango wa Vigae. Ukifika huko, utangaze maneno ninayokuambia.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambazo nafasi hii haitaitwa tena Tofeti, wala bonde la Mwana wa Hinomu, lakini itaitwa bonde la Mauaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Walimujengea mungu Bali mazabahu katika bonde la Mwana wa Hinomu, kusudi wamutolee mungu Moleki wana wao na wabinti zao, ingawa sikuwaamuru wala sikufikiria kwamba wangefanya hivyo. Wakasukuma watu wa Yuda watende zambi.


Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalema, na mpaka leo Wayebusi wangali wanaishi katika muji ule pamoja na watu wa Yuda.


Lakini watu wa kabila la Benjamina hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa katika Yerusalema; ndiyo maana Wayebusi wanakaa pamoja na watu wa kabila la Benjamina katika Yerusalema mpaka leo.


Watu wa kabila la Yuda waliushambulia Yerusalema na kuuteka. Waliwaua wakaaji wake kwa mapanga na kuuteketeza muji kwa moto.


Lakini yule mutu akakataa kulala kule usiku ule. Basi, akasimama, akaondoka, akafika karibu na muji wa Yebusi, ni kusema Yerusalema. Alikuwa na wale punda wake wawili waliotandikwa tayari, pamoja na habara yake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις