Daudi alipofika kwenye kichwa cha mulima, nafasi ya kumwabudia Mungu, mutu mumoja jina lake Husai kutoka inchi ya Arki alikuja kwa kumupokea, nguo zake zikiwa zimepasuka na juu ya kichwa chake kuna mavumbi.
Ahitofeli alikuwa mushauri wa mufalme. Ahitofeli alipokufa, alikombolewa na Yehoyada mwana wa Benaya na Abiatari. Husai Mwarki, alikuwa rafiki ya mufalme. Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi la mufalme.
Inchi zao na makao yao yalikuwa: Beteli na vijiji vyake, muji wa Narani uliokuwa upande wa mashariki, muji wa Gezeri uliokuwa upande wa magaribi pamoja na vijiji vyake, Sekemu na vijiji vyake, na Aya na vijiji vyake.
Kutoka kule, mupaka wake ulikwenda kusini kuelekea Luzi kupitia upande wa kusini wa Luzi, ni kusema Beteli, hata Ataroti-Adari, kwenye mulima unaokuwa upande wa kusini wa Beti-Horoni ya Chini.