Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 15:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya inchi ya Yuda kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriati-Arba au muji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Muji huo sasa unaitwa Hebroni.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 15:13
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Alikufia kule Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana. Abrahamu akaomboleza na kumufanyia Sara muke wake kilio.


Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”


Jamaa za ukoo wa Gersoni walipewa miji hii pamoja na mashamba yake ya malisho: katika nusu ya kabila la Manase walipewa: Golani katika Basani pamoja na mashamba yake ya malisho, Astaroti pamoja na mashamba yake ya malisho.


Zora, Ayaloni na Hebroni. Miji hiyo yenye kuzungukwa kuta iko Yuda na Benjamina.


Lakini Kalebu akanyamazisha watu mbele ya Musa, akasema: Tuende mara moja tuitwae inchi hiyo. Kwa sababu tuko na uwezo sana wa kushinda.


Wakati ule, Yoshua akakwenda, akawaangamiza Waanaki waliokuwa wanaishi katika milima kule Hebroni, Debiri, Anabu, inchi yote ya milima ya Yuda na Israeli. Yoshua akawaangamiza watu hao pamoja na miji yao.


Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.


Wakapewa Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni (Arba alikuwa baba ya Anaki), katika milima ya Yuda, pamoja na mbuga zilizoizunguka.


Waliwashambulia vilevile Wakanana walioishi katika muji wa Hebroni ambao zamani uliitwa Kiriati-Arba, wakashinda makabila ya Sesai, Ahimani na Talmayi.


Muji wa Hebroni ukapewa kwa Kalebu kufuatana na maagizo ya Musa. Kalebu akazifukuza kutoka kule ukoo tatu za Anaki.


Mutu yule aliitwa Nabali na muke wake aliitwa Abigaili. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye akili na sura nzuri. Lakini Nabali alikuwa mutu wa chuki na mutenda maovu; tena alikuwa wa ukoo wa Kalebu.


Sisi tulishambulia Negebu ya Wakereti na eneo la Yuda pamoja na Negebu ya Kalebu. Muji wa Ziklagi tuliuteketeza kwa moto.”


na wakaaji wa Hebroni. Daudi aliwapelekea vilevile wakaaji wa miji yote ambako yeye na watu wake walitembelea.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις