Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 15:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekuroni, ukazunguka kuelekea Sikeroni ambapo ulipita karibu na mulima Bala mpaka Yabuneli ukaishia katika bahari ya Mediteranea.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 15:11
15 Σταυροειδείς Αναφορές  

Akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu ulituma wajumbe kuomba shauri kwa Bali-Zabubu mungu wa Ekuroni sawa vile hakuna Mungu katika Israeli ambaye ungemwomba shauri, basi, hautashuka katika kitanda ambacho umepanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Wakamujibu: “Tumekutana na mutu ambaye alitutuma turudi kukuambia kwamba Yawe amesema hivi: ‘Kwa nini unatuma wajumbe kwa Bali-Zebubu, mungu wa Ekuroni? Hakuna Mungu katika inchi ya Israeli? Hautashuka katika kitanda ulichopanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.


Mupaka wenu wa upande wa magaribi utakuwa bahari ya Mediteranea.


ambako ulipinda upande wa magaribi kuelekea Seiri; ukapita kaskazini ya mulima wa Yerimu, ni kusema Kesaloni, na kuteremuka mpaka Beti-Semesi ambapo ulipita karibu na Timuna.


Mupaka wa upande wa magaribi ulikuwa bahari ya Mediteranea. Ndivyo ilivyokuwa mipaka ya eneo walilopewa watu wa kabila la Yuda kulingana na ukoo zao.


Kutoka hapo, ulielekea kwenye mulima mpaka chemichemi za Nefutoa, mpaka kwenye miji ya mulima wa Efuroni. Hapo mupaka uligeuka na kuelekea Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu,


Watu wa kabila la Yuda vilevile waliteka miji ya Gaza na eneo lake, Askeloni na eneo lake, na Ekuroni na eneo lake.


Halafu watu wa Israeli na watu wa Yuda walianza kupiga kelele za ushindi, wakawafuatilia Wafilistini mpaka Gati, kwenye milango ya muji wa Ekroni, hata Wafilistini walioumizwa katika vita walikufa katika njia tangu Saraimu mpaka Gati na Ekroni.


Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”


Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.


Miji yote ya Waisraeli ambayo Wafilistini waliiteka kati ya Ekuroni na Gati ilirudishiwa kwa Waisraeli. Waisraeli walikomboa inchi yao kutoka kwa Wafilistini. Tena kulikuwa amani kati ya Waisraeli na Waamori.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις