Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 11:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hao, maana kesho, wakati kama huu, nitawaangamiza wote kwa kuwatia katika mikono ya Waisraeli; nanyi mutakata mishipa ya miguu ya farasi wao na kuteketeza magari yao kwa moto.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 11:6
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Daudi aliteka waaskari wapanda-farasi elfu moja na mia saba, na waaskari wa miguu elfu makumi mbili. Kisha Daudi alikata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wa magari ya vita, lakini aliacha farasi wa kutoshelea kwa magari mia moja.


Elisha akamujibu: “Usiogope kwa sababu wanaokuwa pamoja nasi ni wengi kuliko wanaokuwa pamoja nao.”


Kesho muwashambulie wakati watakapokuwa wakipanda Bonde la Sisi. Mutawakuta mwisho wa bonde, upande wa mashariki wa jangwa la Yerueli.


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Mukuje muone matendo ya Yawe. Muone maajabu aliyofanya katika dunia.


Heri watoto wa mutu wa haki mwenye mwenendo mukamilifu!


Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Kwa hiyo, watu wanaoishi katika miji ya Israeli watatoka na kukusanya silaha zilizoachwa na kuzichoma kwa moto. Watatumia hizo ngao, pinde, mishale, mikuki na magongo, kama kuni za kuwasha moto kwa muda wa miaka saba.


Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.


Simba dume amewararulia watoto wake nyama ya kutosha, akiwakamatia simba dike nyama zao; ameyajaza mapango yake na nyama, na makao yake vipande vya nyama.


Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hata kidogo maana nimewatia katika mikono yako, wala hakuna hata mumoja atakayeweza kukushinda.”


Wafalme hawa wote wakaungana na kupiga kambi yao katika chemichemi ya Meromu kusudi wapigane na Waisraeli.


Basi, kwa rafla kwenye chemichemi ya Meromu, Yoshua pamoja na waaskari wake wote akawatokea na kuwashambulia.


Yoshua akakatakata mishipa ya miguu ya farasi wao wote na kuyateketeza magari yao kwa moto, kama Yawe alivyomwagiza.


Yoshua akawaambia watu: “Mujitakase kwa sababu kesho Yawe atatenda maajabu kati yenu.”


Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni alikuwa na kazi ya kutumika mbele yake. Waisraeli wakamwuliza Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, watu wa kabila la Benjamina?” Yawe akawaambia: “Muende. Kesho nitawatia katika mikono yenu.”


Usiku ule, Yawe akamwambia Gideoni: “Kwenda uwashambulie katika kambi yao, maana nimewatia katika mikono yako.


Wakawaambia wale wajumbe waliorudi kutoka Yabesi: “Muwaambie wakaaji wa Yabesi-Gileadi hivi: kesho, wakati jua linapokuwa kali, mutakuwa mumekombolewa.” Watu wa Yabesi walipopata habari hizo walifurahi sana.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις