“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula, lakini mumeacha mambo makubwa yanayoamuriwa na Sheria, kama vile haki, huruma, na uaminifu. Mambo hayo ndiyo muliyopaswa kushika pasipo kuacha mengine.
“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.
Kisha Musa akamwita Yoshua, akamwambia mbele ya watu wote wa Israeli: “Ukuwe imara na hodari, maana wewe utawaongoza watu hawa kwenda kurizi inchi ambayo Yawe aliwaahidi babu zao, nawe utawapatia wairizi.
Ukuwe tu imara na hodari. Ukuwe mwangalifu na kushika sheria yote mutumishi wangu Musa aliyokuamuru. Fuata kila sehemu ya sheria hiyo nawe utafanikiwa popote utakapoenda.
Yoshua aliiteka inchi nzima: sehemu za milima na sehemu zote za kusini, eneo lote la Goseni, inchi ya mabonde, inchi ya Araba, milima ya Israeli na sehemu zake za mabonde;
“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.