Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 11:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Musa mutumishi wa Yawe aliipewa amri hii, naye Musa akamwamuru Yoshua ambaye aliitimiza. Yoshua alitimiza kila jambo Yawe alilomwamuru Musa.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 11:15
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nguvu za Mungu zilikuwa zikifanya kazi katika Yuda, zikitia moyo wa kutii amri za mufalme na wakubwa wake kadiri ya maagizo ya Yawe.


Katika mabonde ya Moabu, ngambo ya muto Yordani karibu na Yeriko, Yawe akamwambia Musa:


muwafukuze wenyeji wote wa inchi hiyo mbele yenu. Mutaziharibu sanamu zao zote za mawe na za kuyeyushwa na kubomoa kila pahali pao pa ibada.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula, lakini mumeacha mambo makubwa yanayoamuriwa na Sheria, kama vile haki, huruma, na uaminifu. Mambo hayo ndiyo muliyopaswa kushika pasipo kuacha mengine.


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Munajua kwamba sikuwaficha hata neno moja lenye kuwafalia ninyi, lakini niliwahubiri na kuwafundisha katika mikutano na katika nyumba zenu.


Ni vile kwa sababu niliwatangazia mupango wote wa Mungu pasipo kuwaficha kitu.


Yawe, Mungu wenu, atawatangulia na kuyaangamiza mataifa yanayoishi huko, kusudi murizi inchi yao. Yoshua atakuwa kiongozi wenu kama vile Yawe alivyosema.


Yawe atawapa ushindi juu yao nanyi mutawatendea kama vile nilivyowaamuru.


Kisha Musa akamwita Yoshua, akamwambia mbele ya watu wote wa Israeli: “Ukuwe imara na hodari, maana wewe utawaongoza watu hawa kwenda kurizi inchi ambayo Yawe aliwaahidi babu zao, nawe utawapatia wairizi.


Musiongeze chochote katika amri ninazowapa, wala musipunguze kitu. Mushike amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa.


“Muangalie! Nimewafundisha masharti na maagizo kama vile Yawe, Mungu wangu alivyoniamuru nifanye, kusudi muyashike katika inchi munayokwenda kuirizi.


Vilevile, kisha Yawe, Mungu wenu, kuyatia katika mikono yenu, mutayashinda na kuyaangamiza kabisa. Musifanye agano lolote nayo wala musiyahurumie.


Ukuwe tu imara na hodari. Ukuwe mwangalifu na kushika sheria yote mutumishi wangu Musa aliyokuamuru. Fuata kila sehemu ya sheria hiyo nawe utafanikiwa popote utakapoenda.


Vilevile aliiteketeza miji ile mingine yote kwa moto na kuwaua wafalme wao wote kama vile Musa, mutumishi wa Yawe, alivyomwamuru.


Waisraeli wakatwaa vitu vyote walivyonyanganya na nyama wa miji hiyo; lakini waliwaua wakaaji wake wote, wala hawakumwacha hata mutu mumoja.


Yoshua aliiteka inchi nzima: sehemu za milima na sehemu zote za kusini, eneo lote la Goseni, inchi ya mabonde, inchi ya Araba, milima ya Israeli na sehemu zake za mabonde;


“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις