Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 10:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 “Mukuje munisaidie tuwaangamize Wagibeoni, maana wamefanya mapatano ya amani na Yoshua pamoja na Waisraeli.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 10:4
15 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Kama mungekuwa watu wa dunia, dunia ingewapenda, kwa maana ninyi ni watu wake. Lakini nimewachagua ninyi toka dunia hii, na ninyi si watu wa dunia tena. Ni kwa sababu hii dunia inawachukia.


wakilalamika: “Ninyi wanainchi Waisraeli, mutusaidie! Huyu ndiye mutu yule anayefundisha kwa watu wote, nafasi zote maneno ya kuzarau taifa letu, Sheria ya Musa, na hekalu hili. Na zaidi ya hii, amewaingiza watu wa mataifa mengine katika hekalu na hivi amechafua Pahali hapa Patakatifu!”


Nao wote wanaotaka kuishi maisha ya kumwabudu Mungu katika kuungana na Kristo Yesu, watateswa.


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


Mufalme Adoni-Zedeki wa Yerusalema akapata habari juu ya jinsi Yoshua alivyouteka muji wa Ai na kuuharibu kabisa akiutendea muji huo na mufalme wake kama alivyoutendea Yeriko na mufalme wake. Vilevile akapata habari kwamba wakaaji wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli na kwamba sasa wanaishi kati yao.


Kisha wafalme hao watano wa Waamori: mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni, mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi na mufalme wa Eguloni, wakaunganisha waaskari wao, wakaenda nao mpaka Gibeoni. Wakapiga kambi kuuzunguka muji huo, wakaushambulia.


Yoshua akafanya nao mapatano ya amani; akafanya agano kwamba atawaruhusu kuishi. Viongozi wa Waisraeli wakawaapia kutimiza mapatano hayo.


Sasa, wapagani wanashangaa kuona ninyi hamushirikiani nao tena katika maisha ya ovyo ovyo; na kwa hiyo wanawasingizia ninyi.


Hawa ndio pepo wanaoonyesha vitambulisho. Nao ndio wanaokwenda kwa wafalme wote wa dunia na kuwakusanya kwa kupigana vita Siku ile kubwa ya Mungu Mwenye Uwezo.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις