Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoshua 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoshua 1:9
33 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mimi niko pamoja nawe, nitakulinda popote utakapoenda na kukurudisha katika inchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapotimiza ahadi niliyokupa.”


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


Yule bwana wake akatambua kwamba Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, na kwamba ndiye aliyefanikisha mambo yote Yosefu aliyofanya.


Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Lakini ninyi mujipe moyo, wala musiregee kwa maana mutapata malipo kwa kazi munayofanya.”


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Musiogope maana mimi nipo pamoja nanyi. Nitawarudisha wazao wenu toka mashariki, nitawakusanya ninyi kutoka magaribi.


Musijiunge nao katika mashauri yao mabaya, wala musiogope yale wanayoyaogopa wala kuwa na hofu.


Akaniambia: Usiogope wewe unayependwa sana, uko salama. Ukuwe imara na hodari. Aliposema nami, nilipata nguvu, nikamwambia: Bwana, umekwisha kuniimarisha; sema kile ulichotaka kusema.


Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli. –Ni ujumbe wa Yawe. Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe! Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Mulipotoka Misri niliwaahidi kwamba nitakuwa pamoja nanyi siku zote. Basi, ningali pamoja nanyi, kwa hiyo, musiogope kitu.


Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?


Muangalie, Yawe, Mungu wenu, ameiweka inchi hii mbele yenu. Basi! Muende, muirizi kama vile Yawe, Mungu wa wazee wenu alivyowaambia. Musiogope wala musifazaike!’


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”


Uwakusanye mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na wakubwa wenu nipate kusema maneno haya wasikie, nayo dunia ishuhudie juu yao.


Kisha Yoshua akawaamuru viongozi wa watu:


Kama vile tulivyomutii Musa katika mambo yote, ndivyo tutakavyokutii wewe; Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na Musa.


Mutu yeyote atakayeasi amri yako au kukataa kutii maneno yako au jambo lolote unalomwamuru, atauawa. Lakini, wewe ukuwe na nguvu na kuwa hodari.”


Yoshua akawaambia: “Musiogope, wala musikuwe na wasiwasi, mukuwe imara na hodari, maana hivi ndivyo Yawe atakavyowatendea waadui zenu ambao mutapigana nao. Kwa hiyo, mukuwe imara na hodari.”


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiwaogope hata kidogo maana nimewatia katika mikono yako, wala hakuna hata mumoja atakayeweza kukushinda.”


Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii, nitaanza kukutukuza mbele ya watu wote wa Israeli kusudi wajue kwamba, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo vilevile nitakavyokuwa pamoja nawe.


Basi, Yawe alikuwa pamoja na Yoshua na sifa zake zikaenea katika inchi yote.


Yawe akamwambia Yoshua: “Usiogope, wala usikuwe na wasiwasi wowote; uwatwae waaskari wako wote uelekee muji wa Ai, maana nimetia mufalme wa Ai katika mikono yako, pamoja na watu wake, muji wake na inchi yake.


Yawe akamugeukia, akamwambia: “Kwenda kwa uwezo unaokuwa nao, uikomboe Israeli kutoka Wamidiani. Ni mimi ninayekutuma.”


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις