Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoeli 2:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Mutapata chakula kingi na kutosheka; mutalisifu jina la Yawe, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoeli 2:26
41 Σταυροειδείς Αναφορές  

Basi, ninakuomba ukubali zawadi niliyokuletea, kwa sababu hata mimi vilevile Mungu amenineemesha, nami nina mali nyingi.” Ndivyo Yakobo alivyomushawishi Esau, naye akapokea zawadi yake.


Wakateka miji yenye kuta, wakatwaa inchi yenye utajiri, nyumba zenye vitu vingi vizuri, visima vilivyochimbwa, mashamba ya mizabibu na mizeituni pamoja na miti yenye matunda kwa wingi. Hivyo wakakula, wakashiba na kunenepa na kufurahia wema wako.


Anajaza maisha yangu na raha, hata ninabaki kijana mwenye nguvu kama tai.


Ukuwe na utulivu mukubwa, ee nafsi yangu, kwa vyote Yawe amenitendea.


Lakini mimi ninatumainia wema wako, moyo wangu ufurahie wokovu wako. Nitakuimbia wewe, ee Yawe, kwa vyote ulivyonitendea!


Kwa sababu yako ninakusifu katika kusanyiko kubwa la watu; nitatimiza ahadi zangu mbele ya wanaomwabudu.


Hawatafezeheka nyakati mbaya zikiwafikia; siku za njaa watakuwa na chakula tele.


Mataifa yote yafurahi na kuimba kwa furaha; maana unawahukumu watu kwa usawa, na kuyaongoza mataifa katika dunia.


Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye peke yake anafanya miujiza.


Mwenye haki yuko na chakula cha kumutoshelea, lakini tumbo la waovu linataabika kwa njaa.


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Wewe, ee Yawe, ndiwe Mungu wangu; nitakutukuza na kulisifu jina lako, kwa maana umetenda mambo ya ajabu; unaitimiza kwa uaminifu na kweli mipango uliyoipanga tangu zamani.


Kwa hiyo, Yawe aliyemukomboa Abrahamu, anasema hivi juu ya wazao wa Yakobo: Wazao wa Yakobo hawatapata haya tena, hawatainamisha vichwa vyao tena kwa ajili ya haya.


Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe, litapata wokovu wa milele. Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.


Inchi itatoa mazao yake nanyi mutakula na kushiba na kuishi mule kwa usalama.


Chakula chenu nitakipunguza hata wanawake kumi watumie mafika moja tu kwa kupika mikate. Watawagawanyia mukate wenu kwa kipimo. Na hata kisha kula mutaendelea kuwa na njaa tu.


Kupepeta ngano kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na mavuno ya zabibu mpaka wakati wa kupanda mbegu. Mutakuwa na chakula tele na kuishi kwa usalama katika inchi yenu.


Mutakula lakini hamutashiba; njaa itazidi kuwa katika tumbo yenu. Mukiweka akiba haitachungwa, na mukichunga kitu nitakiharibu kwa vita.


Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.


Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.


Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa! Vijana wanaume na wanawake watastawi kwa wingi wa ngano na divai mupya.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Kila mutu anayemwamini hatapata haya.”


Nalo tumaini hili si la udanganyifu, kwa sababu Mungu amemimia upendo wake ndani ya mioyo yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.


kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia, ninaweka jiwe la kukwalisha katika Sayuni nalo ni la kuangusha. Lakini yule anayemwamini hatapata haya.”


Ataotesha majani katika mashamba kwa ajili ya ngombe wenu, nanyi mutakula na kushiba.


Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.


Mutavikula mbele ya Yawe, Mungu wenu, pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua. Mutavikula ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi katika miji yenu.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


Mutakula na kushiba, mutamushukuru Yawe, Mungu wenu, kwa inchi nzuri aliyowapa.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις