Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoeli 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Usiogope, ewe inchi, lakini ufurahi na kushangilia, maana Yawe ametenda mambo makubwa.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoeli 2:21
21 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Nguvu na haki yako, ee Mungu, vinafika mpaka juu katika mbingu. Wewe umefanya mambo makubwa sana. Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe?


Enyi mito, mupige vigelegele; enyi vilima, muimbe pamoja kwa shangwe.


Mbuga na inchi kavu vitachangamuka, jangwa litafurahi na kuchanua maua.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.


Nitawaondoa hao waadui wanaotoka kaskazini, nitawafukuza mpaka katika jangwa; waaskari wa mbele nitawatupa katika bahari ya Chumvi na wale wa nyuma katika bahari ya Mediteranea. Watatoa uvundo na harufu mbaya, hao ambao wamefanya maovu makubwa.


Mutapata chakula kingi na kutosheka; mutalisifu jina la Yawe, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


vile vile nimekusudia kuutendea wema Yerusalema na watu wa Yuda. Basi, musiogope.


“Mufikiri sana juu ya matukio ya zamani, mambo yaliyotukia mbele ninyi hamujazaliwa, tangu siku ile Mungu alipomwumba mutu katika dunia. Muulize katika ulimwengu wote, toka pembe moja mpaka nyingine, kama jambo la ajabu la namna hii limepata kutokea au kusikilika!


Kwa hiyo basi, mutulie na kulitazama jambo hilo kubwa ambalo Yawe atatenda mbele yenu.


Basi, ninyi mumutii Yawe na kumutumikia kwa uaminifu, kwa moyo wenu wote. Mukumbuke yale mambo makubwa aliyowatendea.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις