Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoeli 2:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoeli 2:19
21 Σταυροειδείς Αναφορές  

Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.


Nitawapa mashamba yenye mboleo kusudi wasiangamizwe tena na njaa katika inchi ile, wala kuzarauliwa tena na mataifa mengine.


Sitaruhusu tena mataifa yawatukane, wala kuwazarau tena. Hamutasababisha taifa lenu kukosa. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Nitawaokoa kutoka uchafu wenu wote. Nitaiamuru ngano iongezeke, wala sitawaletea njaa tena.


Nitayazidisha matunda ya miti na mazao ya mashamba kusudi musizarauliwe tena kwa ajili ya njaa kati ya mataifa.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Nitamulipiza kwa ajili ya siku alizoabudu sanamu za mungu Bali, kwa ajili ya muda alioutumia kuzifukizia ubani, akajipamba kwa pete zake na ushanga, na kuwaendea wapenzi wake, akanisahau mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.


Kweli, nitakuoa kwa uaminifu, nawe utanijua mimi Yawe.


Mashamba yamebaki matupu. Inchi inaomboleza, maana ngano imeharibiwa, divai imetoweka, mafuta yamekosekana.


Nafasi ya kupepetea itajaa ngano, vikamulio vitafurika divai na mafuta.


Kupepeta ngano kutaendelea mpaka wakati wa kuvuna zabibu, na mavuno ya zabibu mpaka wakati wa kupanda mbegu. Mutakuwa na chakula tele na kuishi kwa usalama katika inchi yenu.


Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


yeye ataipatia inchi yenu mvua wakati wake, mvua za kwanza na mvua za mwisho, nanyi mutavuna ngano yenu, divai yenu na mafuta yenu.


Kisha, Naomi akapata habari kwamba Yawe alikuwa amewabariki watu wake kwa kuwapa chakula. Basi, akaondoka kutoka Moabu kurudi kwao, pamoja na wakwe zake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις