Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoeli 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoeli 1:13
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Daudi alimwomba Mungu kwa ajili ya mutoto yule. Akafunga kula chakula, akaingia ndani ya chumba chake, na usiku kucha akalala chini.


Lakini, Ahabu aliposikia maneno hayo, akapasua nguo zake, akavaa gunia peke yake, akafunga, akakuwa analala na gunia, na kwenda huko na huko kwa huzuni.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Nanyi mutaitwa: “Makuhani wa Yawe”, Mutaitwa: “Watumishi wa Mungu wetu”. Mutafaidika kwa utajiri wa mataifa, mutatukuzwa kwa mali zao.


Kwa hiyo, muvae gunia, muomboleze na kulia; kwa maana Yawe hajaondoa hasira yake kali kwenu.


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Wakikuuliza hivi: Kwa nini unaomboleza? Utawaambia: Ninaomboleza kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila mutu atavunjika moyo, mikono yao yote itaregea; kila mutu anayeishi atazimia na magoti yao yataregea. Habari hizo zinakuja kweli, nazo zinatimia. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.


Watajinyoa vichwa kwa ajili yako na kuvaa gunia. Watalia kwa uchungu wa moyo juu yako.


Watavaa gunia, hofu itawashika, nao watapata haya na vichwa vyao vyote vitanyolewa.


Mutafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa, au katika karamu ya Yawe?


Lakini hata sasa, munirudilie kwa moyo wote, kwa kufunga kula, kwa kulia na kuomboleza. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Labda Yawe, Mungu wenu, atabadilisha nia na kuwapa baraka ya mazao, mutaweza kumutolea sadaka za chakula na kinywaji.


Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?


Kipimo cha sadaka ya kinywaji kinachohitajika ni litre mbili za divai kwa kila ngombe dume; litre moja na nusu kwa kila kondoo dume, na litre moja kwa kila mwana-kondoo. Hii ndiyo sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi katika mwaka muzima.


Mwana-kondoo mumoja atatolewa asubui na wa pili magaribi;


Sadaka ya kinywaji itakayotolewa na kila mwana-kondoo ni litre moja ya divai. Utaimimina sadaka hii ya kinywaji kikali Pahali Patakatifu.


Mutatoa vitu hivi zaidi ya ile sadaka ya kuteketezwa ya mwezi mupya na sadaka yake ya vyakula, na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya vyakula na sadaka zake za kinywaji kama vile inavyoagizwa. Itakuwa harufu nzuri yenye kupendeza; ni sadaka kwa Yawe iliyoteketezwa kwa moto.


Kwa hiyo mutuhesabu kama watumishi wa Kristo, wanaoshugulika na ujumbe wa siri wa Mungu.


Munajua hakika kuwa wale wanaotumika katika hekalu wanapata chakula chao ndani ya hekalu. Na wale wanaotumika kwa kutoa sadaka juu ya mazabahu wanapata sehemu yao kutoka sadaka zile.


Sasa nitasema kama mwenda-wazimu: wao ni watumishi wa Kristo? Mimi ni mutumishi wake zaidi kuliko wao. Nimetumika kazi nyingi zaidi, nimefungwa mara nyingi zaidi, nimepigwa zaidi, na mara nyingi nimekuwa katika hatari ya kufa.


Kwa maana Mungu ndiye aliyetuwezesha kuwa watumishi wa agano jipya, lisilotokana na Sheria iliyoandikwa, lakini na Roho. Sheria iliyoandikwa inaleta kifo lakini Roho analeta uzima.


Lakini tunaonyesha katika mambo yote kwamba sisi ni watumishi wa Mungu: tumedumu sana katika mateso, katika ukosefu na katika taabu.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις