Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 9:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wafarisayo wamoja wakasema: “Mutu huyu hakutoka kwa Mungu kwa sababu hashiki sheria ya siku ya Sabato.” Lakini wengine wakasema: “Mutu mwenye zambi anaweza kuonyesha kitambulisho kama hiki?” Basi kukatokea mikorogano kati yao.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 9:16
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Mule ndani mulikuwa mutu mumoja mwenye mukono unaokauka. Nao watu wamoja waliokuwa pale walitafuta sababu ya kumushitaki Yesu; kwa hiyo wakamwuliza: “Sheria yetu inaruhusu kumuponyesha mutu kwa siku ya Sabato?”


Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakamwambia Yesu: “Angalia! Wanafunzi wako wanafanya mambo yanayokatazwa kufanya kwa siku ya Sabato!”


Lakini mukubwa wa nyumba ya kuabudia alichukizwa kwa sababu Yesu aliponyesha mutu kwa siku ya Sabato. Kwa hiyo akawaambia watu waliokusanyika pale: “Kuna siku sita za kazi. Basi mufike kwa kuponyeshwa katika siku zile, hapana kwa siku ya Sabato!”


Kwa sababu ya maneno haya kukatokea tena mikorogano kati ya Wayuda.


Muniamini wakati ninaposema kama mimi ni ndani ya Baba na Baba ni ndani yangu. Kama si vile, mwamini kwa sababu ya matendo niliyofanya.


Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.


Ni vile Yesu alivyofanya kitambulisho chake cha kwanza katika Kana ya Galilaya. Pale alionyesha utukufu wake na wanafunzi wake wakamwamini.


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


kwa hiyo Wayuda wakamwambia mutu yule aliyeponyeshwa: “Leo ni siku ya Sabato, na Sheria haikuruhusu kubeba kipoyi chako.”


Lakini mimi nina ushuhuda mukubwa zaidi kuliko ule uliotolewa na Yoane. Maana sasa mambo ninayofanya ndiyo Baba aliyoniamuru kutimiza, nayo yananishuhudia na kuonyesha kwamba yeye amenituma.


Basi Wayuda wakaanza kubishana sana kati yao, wakasema: “Namna gani mutu huyu anaweza kutupatia mwili wake tuukule?”


Katika kundi lile kulikuwa manunguniko mengi juu yake. Wamoja walisema: “Yeye ni mutu muzuri.” Wengine walisema: “Hapana, si vile, yeye anawadanganya watu.”


Basi, kama munaweza kutahiri mutu kwa siku ya Sabato, kusudi musivunje Sheria ya Musa, kwa nini munanikasirikia kwa sababu nimemuponyesha mutu kabisa kwa siku ya Sabato?


Basi kukatokea mikorogano katika kundi juu ya Yesu.


Halafu wakubwa wa Wayuda wakamwita yule aliyekuwa kipofu kwa mara ya pili na kumwambia: “Sema ukweli mbele ya Mungu! Kwa ngambo yetu tunajua kwamba mutu yule ni mwenye zambi.”


Watu wa muji wakatengana: wamoja walikuwa upande wa Wayuda na wengine upande wa mitume.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις