Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 8:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Ninyi munafanya matendo yale baba yenu anayofanya.” Wakamujibu: “Sisi si watoto wa haramu. Tuko na baba mumoja, naye ndiye Mungu.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 8:41
17 Σταυροειδείς Αναφορές  

Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


Yawe anasema: Wewe Israeli, mimi niliwaza hivi: heri ningekuhesabia kati ya wana wangu, na kukupa inchi nzuri ajabu, ndio urizi unaopita inchi zote za mataifa. Nilizani utaniita Baba Yako, na kwamba haungeacha kunifuata.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe alipoanza kusema na Waisraeli kwa njia ya Hosea, alimwambia hivi: Kwenda kuoa mwanamuke muzinzi, uzae naye watoto wa uzinzi, maana watu wa inchi hii wanafanya uzinzi mwingi kwa kuniacha mimi.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.


Mimi ninasema yale niliyoona kwa Baba yangu, lakini ninyi munafanya yale muliyosikia kutoka kwa baba yenu.”


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


“Ninyi ni watoto wa Yawe, Mungu wenu; musijichanje wala kunyoa nywele upande wa mbele kwa ajili ya mutu aliyekufa.


Munaweza namna gani kumulipa hivyo Yawe, enyi watu wapumbafu na wasiokuwa na akili? Yeye siye baba yenu aliyewaumba, aliyewafanya na kuwaimarisha?


Tusikuwe kama Kaina aliyekuwa wa yule Mwovu, akamwua ndugu yake. Yeye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις