Vilevile ninawaambia, ndivyo kutakuwa furaha kubwa zaidi mbinguni kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake, kuliko wenye haki makumi tisa na tisa wasiokuwa na lazima ya kugeuka toka zambi zao.
Yesu akajibu: “Ufalme wangu si wa dunia hii. Ufalme wangu ungekuwa wa dunia hii, watumishi wangu wangenipigania kusudi nisitolewe kwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa katika dunia.”
Basi si kazi yangu kuhukumu wale wanaokuwa wa inje ya kanisa. Mungu ndiye atakayewahukumu. Lakini ninyi hamupaswi kuhukumu watu wa kanisa lenu? Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mumwondoe mutu yule mubaya toka katikati yenu.”
Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.