Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, hakuna mutu.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi vilevile sikuhukumu. Ujiendee, lakini usifanye zambi tena.”]

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 8:11
27 Σταυροειδείς Αναφορές  

Labda mutu atamwambia Mungu hivi: “Nimekosa, sitatenda zambi tena.


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Mumutafute Yawe wakati angali anaweza kupatikana, mumwombe musaada wakati angali karibu.


Hakika si vile, lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.


Hakika si vile: lakini musipogeuka toka zambi zenu, ninyi wote mutaangamia kama wao.”


Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”


Kwa hivi ilitupasa kushangilia na kufurahi, kwa maana mudogo wako huyu alikuwa amekufa na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ ”


Vilevile ninawaambia, ndivyo kutakuwa furaha kubwa zaidi mbinguni kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake, kuliko wenye haki makumi tisa na tisa wasiokuwa na lazima ya kugeuka toka zambi zao.


Sikukuja kuwaita wenye haki, lakini wenye zambi kusudi wageuke toka zambi zao.”


Kisha wakaondoka kwenda katika kijiji kingine.


Yesu akajibu: “Ufalme wangu si wa dunia hii. Ufalme wangu ungekuwa wa dunia hii, watumishi wangu wangenipigania kusudi nisitolewe kwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa katika dunia.”


Mungu hakumutuma Mwana wake katika ulimwengu kusudi ahukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe naye.


Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”


Ninyi munahukumu kwa kufuatana na mafikiri ya kimutu; lakini mimi simuhukumu mutu.


Au haujali na uwingi wa wema, utulivu na uvumilivu wa Mungu? Haujui kwamba wema wake ungeweza kukuongoza hata upate kugeuka toka zambi?


Basi si kazi yangu kuhukumu wale wanaokuwa wa inje ya kanisa. Mungu ndiye atakayewahukumu. Lakini ninyi hamupaswi kuhukumu watu wa kanisa lenu? Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mumwondoe mutu yule mubaya toka katikati yenu.”


“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.


na huko mutawaendea makuhani wa Kilawi, na mwamuzi ambaye yuko katika kazi kwa wakati huo, nanyi mutatoa mashitaki kwao nao watawatangazia uamuzi wao.


Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις