Lakini wakati walimaji walipomwona yule mwana, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue, na shamba hili litakuwa urizi wetu!’
Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walipopata habari hii, wakatafuta njia ya kumwua Yesu. Lakini walimwogopa, kwa sababu kundi lote la watu walishangaa na mafundisho yake.
Kwa ajili ya neno hili Wayuda walitaka tena zaidi kumwua; si kwa sababu ya kuvunja Sheria ya siku ya Sabato tu, lakini vilevile kwa sababu alisema kwamba Mungu ni Baba yake, akijifanya hivi kuwa sawasawa na Mungu.
Na wakati ule kulipokuwa mukutano wa Waisraeli katika jangwa, yeye alikuwa pale pamoja na babu zetu na yule malaika aliyesema naye kwenye mulima Sinai. Na ni yeye aliyefunuliwa ujumbe wa Mungu unaoleta uzima na kuutangaza kwetu.
Basi Sheria iko na kazi gani? Ilisimamishwa nyuma kwa ajili ya kutambulisha makosa. Nayo ilipaswa kuendelea mpaka atakapokuja yule muzao wa Abrahamu ambaye Mungu alikuwa ameahidi. Sheria hii ilitangazwa na malaika kwa njia ya mupatanishi.
Watu hao wanaotahiriwa, hawashiki Sheria lakini wanataka mutahiriwe kusudi wapate kujivuna kwamba wanawashurutisha kuwa na kitambulisho kile juu ya mwili wenu.
Musipendelee mutu yeyote katika kutoa hukumu; mutawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Musiogopeshwe na sura ya mutu, maana ninyi mutapaswa kuhukumu kwa ajili ya Mungu. Kukikuwa maneno ambayo ni magumu sana kwenu, mutayafikisha kwangu nami nitayasikiliza.’