Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 7:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 7:17
25 Σταυροειδείς Αναφορές  

Ninakutafuta kwa moyo wote; usiniachilie kugeuka mbali na amri zako.


Kila mutu anayemwabudu Yawe, Yawe atamufundisha njia ya kufuata.


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Waovu hawaelewi haki ya sheria, lakini wanaomwogopa Yawe wanaielewa kabisa.


Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Watu wengi wataondolewa uchafu, watatakaswa na kusafishwa. Lakini watu waovu wataendelea kutenda uovu. Hakuna hata mumoja wa hao waovu atakayeelewa; wenye hekima ndio watakaoelewa.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.


“Macho ni taa ya mwili. Kama macho yako yakiwa mazima, mwili wako wote utabaki katika mwangaza.


Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Lakini anayeshika ukweli, anakuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yaonekane wazi kwamba yanatendeka sawa Mungu anavyoamuru.”


Kwa sababu gani hamuelewi maneno ninayowaambia? Ni kwa sababu hamutaki kusikia maneno yangu.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Anayekuwa mutu wa Mungu anasikia maneno ya Mungu. Hamusikii, kwa sababu ninyi si watu wa Mungu.”


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις