Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 6:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Basi Wayuda wakaanza kubishana sana kati yao, wakasema: “Namna gani mutu huyu anaweza kutupatia mwili wake tuukule?”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 6:52
11 Σταυροειδείς Αναφορές  

Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.


Kwa sababu ya maneno haya kukatokea tena mikorogano kati ya Wayuda.


Nikodemo akamwuliza: “Namna gani mutu anaweza kuzaliwa akiwa muzee? Anaweza kurudi ndani ya tumbo la mama yake na kuzaliwa mara ya pili?”


Basi Nikodemo akamwuliza: “Maneno haya yanawezekana namna gani?”


Yule mwanamuke akamwambia: “Bwana, hauna chombo cha kutekea, na kisima ni kirefu sana. Basi umepata wapi maji ya uzima?


Basi Wayuda wakaanza kunungunika kwa sababu Yesu alisema kwamba yeye ni mukate ulioshuka toka mbinguni.


Wengi kati ya wanafunzi wake waliposikia maneno haya, wakasema: “Masemi haya ni magumu. Ni nani anayeweza kuyakubali?”


Wafarisayo wamoja wakasema: “Mutu huyu hakutoka kwa Mungu kwa sababu hashiki sheria ya siku ya Sabato.” Lakini wengine wakasema: “Mutu mwenye zambi anaweza kuonyesha kitambulisho kama hiki?” Basi kukatokea mikorogano kati yao.


Nao waliposikia Paulo akisema juu ya ufufuko, wamoja wakamuchekelea na wengine wakasema: “Tutakusikiliza tena ukisema juu ya habari hii siku ingine.”


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις