Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 5:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Na zaidi ya hii Baba hahukumu hata mutu mumoja, lakini amemupa Mwana uwezo wote wa kuhukumu,

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 5:22
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake.


Mushangilie mbele ya Yawe, maana anakuja kutawala dunia. Atahukumu ulimwengu kwa haki, atatawala mataifa kama vile inavyofaa.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


Vilevile amemupa Mwana mamlaka ya kuhukumu, kwa sababu yeye ni Mwana wa Mutu.


Kisha Yesu akasema: “Nimekuja katika dunia kusudi hukumu ipate kufanyika; maana yake vipofu wapate kuona, nao wanaoona wapate kuwa vipofu.”


Akatuagiza kutangaza Habari Njema kwa watu na kushuhudia kwamba ni yeye aliyewekwa na Mungu kuwa Mwamuzi wa wazima na wafu.


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Hiyo ndiyo itakayotokea siku ile Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya watu kwa njia ya Yesu Kristo, kama vile Habari Njema yangu inavyosema.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


Ninakuamuru mbele ya Mungu na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu wazima na wafu na kufuatana na kurudi kwake kwa kutawala:


Lakini watu hawa watasamba maneno yao mbele ya Mungu anayekwisha kuwa tayari kwa kuhukumu wafu na wazima.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις