Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 5:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Basi Yesu akaongeza kuwaambia Wayuda: “Kweli, kweli, ninawaambia: Mwana hawezi kufanya kitu kwa mafikiri yake mwenyewe; anafanya tu kile ambacho anaona Baba akifanya. Na mambo yote Baba anayofanya, Mwana anayafanya vilevile.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 5:19
43 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kwa maana sikusema kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba aliyenituma ndiye aliyeniagiza maneno nitakayosema na kuyafundisha.


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Hauamini kwamba mimi na baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu na mimi ndani yake? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba anayekaa ndani yangu ndiye anayefanya kazi zake.


Hakuna mutu anayeweza kunionodoa uzima, lakini ninajitoa mwenyewe kufa kwa mapenzi yangu. Niko na uwezo wa kujitoa kufa na niko na uwezo wa kuwa tena muzima. Ni vile Baba yangu alivyoniagiza kufanya.”


Na kama Roho wa Mungu aliyemufufua Yesu anakaa ndani yenu, basi huyo aliyemufufua Kristo ataupatia mwili wenu unaokuwa wa kufa uzima kwa njia ya Roho wake anayekaa ndani yenu.


Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Kwa maana kama vile Baba anavyofufua wafu na kuwarudishia uzima, vile vile Mwana anawapa uzima wale anaowataka.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


Maana Yawe anawapa watu hekima; katika kinywa chake kunatoka maarifa na ufahamu.


Nilipokulilia, wewe ulinijibu; umeniongezea nguvu yangu.


Mbingu zinatangaza haki ya Mungu; Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi.


Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


Kwa njia yake, Mungu aliumba vitu vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia, vyenye kuonekana na visivyoonekana; ikiwa ni ufalme, ukubwa, utawala au mamlaka. Mungu aliumba vyote kwa njia yake na kwa ajili yake.


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Yeye atabadilisha huu mwili wetu wa uzaifu na kuufananisha na mwili wake wa utukufu kwa nguvu ambayo kwa njia yake anaweza kuwa na mamlaka juu ya vitu vyote.


Ninaomba Mungu, kwa uwingi wa utukufu wake, awajalie nguvu mupate kuwa imara ndani ya roho zenu, kwa njia ya Roho wake.


sisi tuliokuwa tumekufa kwa sababu ya makosa yetu, alitufufua pamoja na Kristo. Hivi mumeokolewa kwa neema ya Mungu.


Tunajua kwamba Mungu aliyemufufua Bwana Yesu atatufufua sisi vilevile pamoja na Yesu. Yeye atatufikisha pamoja nanyi mbele ya Yesu.


Ikiwa tunahubiri kuwa Kristo amefufuka, namna gani basi wengine kati yenu wanasema kama wafu hawatafufuka?


Hivi, kwa njia ya ubatizo, tuliungana naye katika kufa na katika kuzikwa kwake, kusudi kama vile Kristo alivyofufuliwa kwa uwezo wenye utukufu wa Baba, sisi vilevile tupate kuishi katika maisha mapya.


Lakini Mungu alimufufua, akimufungua toka vifungo vya lufu, kwa sababu haikuwezekana afungwe na lufu.


Yesu akawajibu: “Mubomoe hekalu hili, nami nitalijenga katika siku tatu.”


Yawe, Mukombozi wako, aliyekuumba tangu katika tumbo, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe niliyeumba vitu vyote. Mimi peke yangu nilizitandaza mbingu, niliiumba dunia kwa nguvu yangu mwenyewe!


Halafu Yawe akamwuliza: “Ni nani aliyeumba kinywa cha mutu? Ni nani anayemufanya mutu kuwa bubu au kiziwi? Aone au akuwe kipofu? Si mimi Yawe?


Tunaamini kwamba Yesu alikufa na alifufuliwa, na kwa hiyo tunaamini vilevile kwamba Mungu atawafufua pamoja na Yesu wale waliokufa wakimwamini Yesu.


Watasema juu yangu: Haki na nguvu viko kwa Yawe peke yake. Wote waliomukasirikia Yawe watakuja kwake na haya.


Mungu atawatia nguvu kwa uwezo wake wenye utukufu, kusudi mupate kuvumilia kila kitu pasipo kuchoka. Basi kwa furaha,


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Nami ninajua kama amri yake inaleta uzima wa milele. Ni kwa hiyo maneno ninayosema, ninayasema tu kama vile Baba alivyoniagiza.”


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις