52 Halafu akawauliza saa gani mutoto alipoanza kujisikia vizuri. Nao wakamujibu: “Yeye alipona homa jana muchana saa saba.”
Yesu akamukaripia yule pepo aliyekuwa ndani ya yule mutoto, naye akamwacha, na tangia saa ile ile yule mutoto akapona.
Kisha Yesu akamwambia yule mukubwa wa waaskari hivi: “Urudie kwako, na ifanyike kwako sawa ulivyoamini.” Na saa ile ile mutumishi wake akapona.
Alipokuwa katika njia akirudi kwake, watumishi wake wakakuja kukutana naye na kumwambia kwamba mutoto wake ni muzima.
Basi baba yule akatambua kama ilikuwa ni saa ile ile Yesu alipomwambia kwamba mwana wake ni muzima. Basi yeye na jamaa yake yote wakamwamini Yesu.