Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 3:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Lakini anayeshika ukweli, anakuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yaonekane wazi kwamba yanatendeka sawa Mungu anavyoamuru.”

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 3:21
31 Σταυροειδείς Αναφορές  

Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.


Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.


kwa maana matunda ya mwangaza ni wema wa kila namna, haki na ukweli.


Neno lako ni taa ya kuniongoza, na mwangaza katika njia yangu.


kwa maana Mungu anafanya kazi ndani yenu na kuwapa moyo wa kutaka na kutimiza mambo yanayolingana na mupango wake mwema.


Anayepanda kwa kupendeza hali yake ya kimwili, atavuna matunda yanayotokana na hali ile, nayo ni lufu. Lakini anayepanda kwa kupendeza Roho Mutakatifu, atavuna matunda yanayotokana na Roho yule, nayo ni uzima wa milele.


Moyo wangu ukuwe mukamilifu juu ya masharti yako, kusudi nisifezeheke.


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Ni kwa sababu hiyo ninatumika na kupigana kwa uwezo ninaopewa na Kristo, unaoniwezesha kufanya kazi kwa nguvu.


Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.


Munachunguza Maandiko Matakatifu, kwa maana munazani kuwa ndani yao mutapata uzima wa milele. Maandiko hayo ndiyo yanayonishuhudia,


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu, watastawi kama bustani nzuri. Watachanua kama muzabibu, harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.


Wewe, ee Yawe, umetupatia amani; umefanikisha shuguli zetu zote.


Ninajua matendo yako: wewe si baridi wala si moto. Afazali ungekuwa baridi tu au moto tu.


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Kila mutu anayefanya mabaya anachukia mwangaza, naye anakataa kuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yasionekane wazi.


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις