Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 19:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Akaingia tena katika nyumba yake na kumwuliza Yesu: “Wewe ni muzaliwa wa wapi?” Lakini Yesu hakumujibu neno.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 19:9
18 Σταυροειδείς Αναφορές  

Alionewa na kuteswa, lakini alivumilia kwa unyenyekevu, bila kutoa sauti hata kidogo. Alikuwa kama mwana-kondoo anayepelekwa kwenda kuchinjwa, kama kondoo anavyokaa kimya anapokatwa manyoya. Hakutoa sauti hata kidogo.


Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”


Kisha waaskari wa liwali Pilato wakamupeleka Yesu ndani ya upango wa nyumba ya liwali, nalo kundi lao lote wakakusanyika na kumuzunguka.


Akamwuliza Yesu maneno mengi, lakini yeye hakumujibu neno.


Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.


Halafu Pilato akarudi ndani ya nyumba, akamwita Yesu na kumwuliza: “Wewe ni mufalme wa Wayuda?”


Yesu akajibu: “Unasema hivi kutokana na mawazo yako mwenyewe au watu wengine wamekuambia habari zangu?”


Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”


Basi Pilato akamwambia: “Hautaki kusema nami? Wewe haujui kama mimi nina mamlaka ya kukufungua na mamlaka ya kukutundika juu ya musalaba?”


Pilato aliposikia neno hili, akazidi kuogopa.


Yesu akawajibu: “Hata nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushuhuda wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua pahali nilipotoka na pahali ninapokwenda. Lakini ninyi hamujui pahali nilipotoka wala pahali ninapokwenda.


Musiogope waadui zenu hata kidogo. Hii itakuwa kitambulisho kwao kwa kuhakikisha kwamba wanapotea, lakini kwenu ni kwamba munaokolewa. Na hii inatoka kwa Mungu.


Mwanamuke huyo akaenda kumwambia mume wake: “Mutu wa Mungu ambaye sura yake ilikuwa kama ya malaika wa Mungu alinitokea. Sikumwuliza anatoka wapi wala hakuniambia jina lake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις