Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 15:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 15:7
24 Σταυροειδείς Αναφορές  

Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”


basi, ndipo utakapomufurahia Mungu Mwenye Uwezo na kuinua uso wako kwake.


Sijaacha hata kidogo kushika amri yake; maneno yake nimeyatunza ndani ya moyo wangu.


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.


Kitu mutu mwovu anachoogopa ndicho kitakachomupata, lakini kitu mwenye haki anachotamani ndicho atakachopewa.


Baba yangu alinifundisha hiki: “Shika kwa moyo maneno yangu, shika amri zangu nawe utaishi.


Mukifanya hivyo mutaonekana kama mwangaza wa mapambazuko, na mutapona haraka. Matendo yenu mema yatawatangulia, nami nitawalinda kutoka nyuma kwa utukufu wangu.


Palepale maneno yako yaliponifikia, niliyameza; nayo yakanifurahisha, yakakuwa matamu katika moyo wangu, maana mimi ninajulikana kwa jina lako, ee Yawe wa majeshi.


“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.


Nami nitafanya chochote mutakachoomba kwa jina langu, kusudi Baba atukuzwe kwa njia ya Mwana.


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


“Siku ile itakapotimia, ninyi hamutaniuliza juu ya kitu fulani. Kweli, kweli ninawaambia: Baba atawapa chochote mutakachomwomba kwa jina langu.


Basi Yesu akawaambia wale Wayuda waliomwamini: “Kama mukitii mafundisho yangu, ninyi ni wanafunzi wangu hakika.


Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu munakataa kukubali mafundisho yangu.


Kwa muda ule yeye ni chini ya madaraka ya watu wanaomuchunga na ya walinzi wa mali mpaka wakati baba yake aliopanga upate kutimia.


Mambo ninayotaka kusema ni haya: muishi chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu, nanyi musitimize tamaa za kimwili.


Muweke ndani ya moyo wenu maneno hayo ninayowaamuru leo


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Nimewaandikia ninyi watoto, kwa sababu mumemujua Baba. Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangia mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu muko na nguvu na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mumemushinda yule Mwovu.


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Nasi tuko na tumaini hili mbele ya Mungu: tunajua kwamba atatusikiliza tukimwomba kitu chochote kufuatana na mapenzi yake.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις