Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 14:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yesu akajibu: “Filipo, nimekwisha kuwa nanyi siku nyingi sasa, nawe haujanijua bado? Aliyeniona mimi amemwona Baba. Basi sababu gani unasema: ‘Utuonyeshe Baba?’

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 14:9
16 Σταυροειδείς Αναφορές  

Abimeleki akamwita Isaka na kumwambia: “Hakika huyo ni muke wako! Sababu gani ulisema kwamba ni dada yako?” Isaka akajibu: “Kwa sababu niliogopa kwamba ningeuawa kwa sababu yake.”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Yawe ni kimbilio langu; namna gani basi munaweza kuniambia: “Ruka kama ndege, mpaka kwenye milima,


Namna gani basi unaweza kusema: Mimi sikujichafua wala sikufuata miungu Bali. Ukumbuke vile ulivyotenda zambi kule katika bonde; utambue yale uliyofanya huko! Wewe ni kama mwana wa ngamia, anayetangatanga huko na huko;


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Ninyi wanafiki! Munajua kutambua hali ya inchi na ya anga, namna gani munashindwa kutambua nyakati hizi za sasa?


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”


Anayeniona amemwona vilevile yule aliyenituma.


Na wakati ule mutafahamu kwamba mimi ni ndani ya Baba yangu, na ninyi ni ndani yangu, na mimi ndani yenu.


Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile. Na tangu sasa mumemujua, na mumemwona.”


Basi wakamwuliza: “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu: “Hamunijui mimi wala hamumujui Baba yangu. Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile.”


Ikiwa tunahubiri kuwa Kristo amefufuka, namna gani basi wengine kati yenu wanasema kama wafu hawatafufuka?


Tangu mwanzo yeye alikuwa na hali ya Mungu, lakini hakuona kwamba kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho.


Kristo ni mufano kamili wa Mungu asiyeonekana. Yeye ni muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις