Biblia Todo Logo
Διαδικτυακή Βίβλος

- Διαφημίσεις -




Yoane 10:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Anapokwisha kuwatia hao kondoo wake inje, anawatangulia, nao wanamufuata kwa sababu wanajua sauti yake.

Δείτε το κεφάλαιο αντίγραφο




Yoane 10:4
23 Σταυροειδείς Αναφορές  

Hiyo ni sauti ya mupenzi wangu, yeye anakuja mbio, anaruka milima, vilima anavipita haraka!


Nililala usingizi, lakini moyo wangu ulikesha. Nikasikia mupenzi wangu akipiga hodi. Unifungulie dada, ee mupenzi wangu, muchumba wangu, njiwa yangu, usiyekuwa na kilema chochote. Kichwa changu kimelowana na umande na nywele zangu na manyunyu ya usiku.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kama mutu akitaka kunifuata, ajikane yeye mwenyewe, lakini ajitolee kwa kubeba musalaba wake na kunifuata.


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


Kondoo wangu wanasikia sauti yangu, ninawajua, nao wananifuata.


Zamu anamufungulia mulango na kondoo wanasikia sauti yake. Naye anawaita kondoo wake kila mumoja kwa jina lake na kuwapeleka inje.


Kondoo wale hawawezi kumufuata mugeni; lakini watamukimbia, kwa sababu hawajui sauti ya mugeni.”


Wote waliokuja mbele sijafika ni wizi na wanyanganyi; lakini kondoo hawakuwasikia.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Mimi nimewapa ninyi mufano, mufanye sawasawa nilivyowafanyia.


Halafu Pilato akamwuliza: “Ni kusema wewe ni mufalme?” Yesu akamujibu: “Wewe umesema kwamba mimi ni mufalme. Mimi nimezaliwa na kuja katika dunia kusudi nishuhudie ukweli. Wote wanaokuwa upande wa ukweli, wananisikiliza mimi.”


Mwenye bibi arusi ndiye bwana-arusi; lakini rafiki ya bwana arusi anasimama karibu naye na kumusikiliza, anafurahi sana kusikia sauti ya bwana-arusi. Na ni hivi mimi ninafurahi, na furaha yangu imetimia sasa.


Mufuate mufano wangu kama vile mimi ninavyofuata mufano wa Kristo.


Mufuate tabia ya Mungu kwa maana ninyi ni watoto wake wapendwa.


Yawe, Mungu wenu, ambaye anawatangulia, yeye mwenyewe atapigana kwa ajili yenu kama vile alivyofanya mbele yenu kule Misri na


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Yesu alitangulia kuingia pahali pale kwa ajili yetu. Amekuwa Kuhani Mukubwa hata milele, kwa mufano wa Melkisedeki.


Ni kwa ajili ya shabaha hiyo Mungu aliwaita kumufuata, kwa sababu Kristo vilevile aliteswa kwa ajili yenu, akiwaachia mufano, kusudi mufuate njia yake.


Kristo aliteswa kimwili. Basi ninyi vilevile mujikaze mupate kuwa na nia kama ile yake. Kwa maana mutu anayevumilia mateso ya mwili, anaachana kabisa na zambi.


Musitawale kwa kinguvu kundi lile lililowekwa chini ya uangalizi wenu, lakini mukuwe mifano kwao.


Ακολουθησε μας:

Διαφημίσεις


Διαφημίσεις