Yoane 10:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.
Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.
Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.
Kweli, kondoo walisambazwa, wakatangatanga juu ya milima na vilima. Kondoo walisambazwa katika dunia yote, na hakukukuwa mutu aliyejali juu yao wala kuwatafuta.
Nitawafanya kuwa taifa moja katika inchi juu ya milima ya Israeli; mufalme mumoja atakuwa mufalme wao wote. Hawatakuwa tena mataifa mawili wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.
“Vilevile ni mwanamuke gani anayekuwa na vikoroti kumi vya feza, naye akipoteza kimoja, atakayekosa kuwakisha taa na kufagia nyumba kutafuta vizuri mpaka akipate?
Simoni anatoka kutuelezea namna Mungu alivyowashugulikia watu wa mataifa mengine pale mbele kusudi ajichagulie wamoja kati yao kuwa watu wake wa pekee.
kwa maana mimi ni pamoja nawe. Hakuna mutu katika muji huu atakayesubutu kukukamata kwa kukutendea vibaya, kwa maana ndani yake kutakuwa watu wengi watakaonigeukia.”
Kisha akasema: ‘Mungu wa babu zetu amekwisha kukuchagua wewe kusudi ujue mapenzi yake. Anataka umwone Mwenye Haki, na kumusikia akisema kwa kinywa chake mwenyewe.
Wandugu zangu, sitaki mukose kujua siri hii, kusudi musijione kuwa wenye akili sana. Siri ile ni hii: Waisraeli wamoja wataendelea kuwa wagumu mpaka watu wa mataifa mengine kwa jumla watakapokuja kwa Mungu.
Lakini sisi tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wandugu wapendwa wa Bwana. Kwa maana Mungu amewachagua ninyi wa kwanza kuwa watu wake kusudi mupate kuokolewa kwa kutakaswa na Roho Mutakatifu na kwa kuamini maneno ya ukweli.
Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.